Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari Kocha Mbeya Kwanza afungiwa miaka mitano
HabariMichezo

Kocha Mbeya Kwanza afungiwa miaka mitano

Spread the love

 

KOCHA wa klabu ya Mbeya Kwanza inayoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara, Mbwana Makata pamoja na meneja wa kikosi hiko David Naftari wamefungiwa miaka mitano kila mmoja kufuatia kuwashawishi wachezaji wao kugomea mchezo wao dhidi ya Namungo FC. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Mchezo huo namba 180, kati ya Namungo dhidi ya Mbeya Kwanza ulishindwa kufanyika kufuatia klabu ya Mbeya kwanza kugomea mchezo kwa kigezo cha kutokuwepo Uwanjani kwa gari la kubebea wagonjwa (Ambulance) kanuni ya 17 inavyoeleza.

Gari hilo lilikuja Uwanjani kwa kuchelewa kwenye majira ya saa 10:24, lakini benchi la ufundi la klabu hiyo ya Mbeya Kwanza halikuingiza timu uwanjani kwa kigezo cha muda kupita.

Mara baada ya mchezo huo, kamati ya uendeshaji na usimamizi wa Ligi (kamati ya saa 72), katika kikao chao, waligundua kwamba viongozi hao walifanya makosa kiasi cha kuwachukulia hatua hizo.

Aidha katika hatua nyingine kamati ya saa 72 iliwapa ushindi klabu ya Namungo wa alama tatu na mabao matatu, kufuatia klabu ya Mbeya Kwanza kufanya kosa hilo la kikanuni.

Klabu hiyo imekosa alama tatu huku ikiwa ya mwisho kwenye masimamo wa Ligi Kuu Tanzania  Bara, ambayo imebakisha michezo saba kuelekea ukingoni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!