Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Kocha atoboa siri ya ushindi Biashara United
Michezo

Kocha atoboa siri ya ushindi Biashara United

Spread the love

 

KOCHA wa kikosi cha Biashara United, Moses Odhiambo amesema kuwa ubora wa wachezaji wake ndio siri kubwa ya kupata ushindi dhidi ya Al Ahly Tripoli ya kutoka nchini Misri. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Mchezo huo wa Kombe la Shirikisho Barani Afrika, ulimalizika kwa Biashara United kuibuka na ushindi wa mabao 2-0.

Mara baada ya mchezo huo, kocha huyo ambaye pia ni mchezaji wa zamani wa Timu ya Taifa ya Kenya (Harambee Stars) alifungukuwa kuwa, siri ya kuondoka na ushindi kwenye mchezo huo ni ubora wa wachezaji wake, licha ya kukili kuwa wapinzani wao wanatimu nzuri.

“Wachezaji wangu walikuwa bora, wapinzani wetu wanatimu nzuri, ila niliona kitu cha wachezaji wangu kutaka kushinda mechi hii.” Alisema Odhiambo

Mabao ya Biashara United kwenye mchezo huo, yalipachikwa kambani na Deogratius Mafie, kwenye dakika 40 ya mchezo, huku bao la pili likifungwa na Atupele Green, dakika ya 62 ya mchezo.

Aidha kocha huyo aliendelea kufunguka  kuwa, bado kazi haijamalizika kwa kuwa wanamchezo wa marudiano hivi karibuni.

“Hatujamaliza, kwa kuwa wapinzani wetu wanaonekana kuwa na timu nzuri sana, na wakiwa nyumbani kwa wanakuwa bora sana.” Alisema Kocha huyo.

Mchezo huo wa marudiano wa utapigwa nchini Libya, Oktoba 24, 2021 ambapo Biashara United wanahitaji ushindi au sare ya aina yoyote ili waweze kusonga mbele kwenye hatua inayofuata.

Biashara United wanashiriki michuano hii kwa mara ya kwanza, toka walipopanda kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara na kumaliza nafasi ya nne kwenye msimu uliomaliza.

Mara baada ya mchezo huo, kikosi cha Biashara kitasafiri kuelekea Sumbawanga, ambapo Oktoba 19, 2021 kitashuka dimbani kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Tanzania Prisons.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!