Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Michezo KMC yatua Arusha kibabe
Michezo

KMC yatua Arusha kibabe

KMC
Spread the love

 

KIKOSI cha KMC imetua jijini Arusha kwa maandaizi ya michezo yake miwili ya Ligi Kuu ya NBC, msimu wa 2022/23 itakayopigwa tarehe 17 na 21 Agosti, mwaka huu katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid uliopo jijini humo. Anaripoti Damas Ndelema, TUDARCo … (endelea).

Timu hiyo ilioyo chini ya kocha, Thiery Hitmana imeondoka jana ikiwa na jumla ya wachezaji 24 huku nyota wake watatu wapya wakisalia jijini Dar es Salaam na wataukosa mchezo huo baada ya kupata majeraha wakati wakiwa mazoezini na wachezaji hao ni Blaise Bigrimana, Waziri Junior, na Eric Manyama

Kupitia taarifa iliyotolewa na Afisa habari na Mawasiliano wa KMC, Christina Mwagala amesema kuwa wamejiandaa vya kutosha na wamekuja Arusha kwa ajili ya kuchukua alama sita katika michezo yote miwili aidha pia wanafahamu kuwa ushindani ni mkubwa kutokana na kila timu imejiandaa vya kutosha.

“Tumekuja kupata alama sita kwenye michezo hii miwili tunajua ushindani ni mkubwa kutokana na jinsi timu zilivyo jiandaa pia tunahitaji ushindi kwa ni jambo ambalo lipo ndani ya uwezo wetu,” alisema Afisa huyo.

Aidha hapo awali kwa mujibu wa ratiba KMC ilitakiwa kuanzia ugenini katika uwanja wa mkwakwani dhidi ya Coastal Union kisha kusafiri mpaka Moshi kucheza na Polisi Tanzania katika uwanja wa Ushirika lakini kutokana na taarifa ya kufungiwa kwa viwanja hivyo ikapelekea kupangwa katika uwanja huo wa Sheikh Amri Abed uliopo jijini Arusha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!