Tuesday , 30 May 2023
Home Kitengo Michezo KMC yaipeleka Yanga CCM Kirumba
Michezo

KMC yaipeleka Yanga CCM Kirumba

Lamine Moro
Spread the love

TIMU ya KMC inayoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara imehamishia mchezo wake wa nyumbani dhidi ya klabu ya Yanga kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza kama walivyopendekeza baada ya mabadiliko ya ratiba. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mchezo huo namba 70 unatarajiwa kuchezwa 25 Oktoba, 2020 majira ya saa 10 jioni kwenye dimba la CCM Kirumba.

Kwa kawaida KMC hucheza michezo yake ya nyumbani ya Ligi Kuu kwenye Uwanja wa Uhuru, Jijini Dar es Salaam lakini mchezo wao dhidi ya Yanga watauhamishia Mwanza kutokana na kanuni kuruhusu timu kuchagua mechi mbili ambazo watacheza kwenye uwanja wa chaguo lao tofauti na uwanja wa nyumbani.

KMC kwa sasa inashika nafasi ya saba kwenye msimamo wa Ligi ikiwa na pointi 9, mara baada ya kucheza michezo mitano huku akishinda mechi tatu na kufungwa mbili.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

NBC Dodoma Marathon yazinduliwa, wakiambiaji 6,000 kushiriki

Spread the loveBENKI ya NBC imetangaza kufanyika kwa mbio kubwa za NBC...

Michezo

Rais Samia anunua tiketi 5000 Yanga vs USM Alger

Spread the loveRAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu...

Michezo

Mwenyekiti UVCCM anogesha nusu fainali Kimwanga CUP, Hawa Abdul Rede CUP kwa kishindo

Spread the loveHEKAHEKA za michuano ya kuwania kuingia fainali ya michuano ya...

Michezo

Yanga SC. yatwaa ubingwa wa pili mfululizo

Spread the love  KLABU ya Yanga SC imeweka rekodi ya kutwaa ubingwa...

error: Content is protected !!