Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Michezo KMC warudisha Dar mchezo wao dhidi ya Simba
Michezo

KMC warudisha Dar mchezo wao dhidi ya Simba

Spread the love

 

Klabu ya KMC ya jijini Dar es Salaam, imerejesha mchezo wake dhidi ya Simba jijini Dar es Salaam, kwenye dimba la Benjamin Mkapa, badala ya CCM Kirumba, Mwanza kama ilivyopangwa hapo awali. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mchezo huo, utapigwa tarehe 7 Julai, 2021, licha ya uongozi wa klabu hiyo kutoeleza sababu za msingi, kurudisha mchezo huo Dae es Salaam.

Licha ya kutumia Uwanja wa Uhuru katika michezo yao ya Ligi Kuu Tanzania Bara, KMC walitangaza kupeleka michezo yao dhidi ya Simba na Yanga kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.

Katika kutekeleza hilo, mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu ambao KMC walikuwa nyumbani dhidi ya Yanga, uliochezwa tarehe 25 Oktoba, 2020, kwenye Uwanja wa CCM Kirumba na Yanga kuibuka na ushindi wa mabao 2-1.

Kikosi hiko chenye maskani yake Kinondoni, Dar es Salaam kimesalia na michezo mitatu kabla ya kukamilika kwa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2020/21, ambayo ni dhidi ya Simba, JKT Tanzania pamoja na Ihefu.

Kwenye mchezo wamzunguko wa kwanza, ambapo timu hizo mbili zilikutana, kwenye Uwanja wa Mkapa tarehe 16 Desemba, 2020, Simba ilifanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!