Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Klopp: Tumepoteza mchezo ambao hatukustahili kupoteza
Michezo

Klopp: Tumepoteza mchezo ambao hatukustahili kupoteza

Jorgen Klopp, Kocha wa Liverpool
Spread the love

KICHAPO cha bao 1-0, dhidi ya Burnley, kocha kikosi cha Liverpool, Jurgen Klopp amesema kuwa timu yake imefungwa kwenye mchezo ambao hawakustahili kufungwa huku akiongezea kuwa hauwezi kufikiria swala la ubingwa kwa sasa. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam …  (endelea).

Mkwaju wa penalti wa Ashley Barnes dakika ya 83, ilitosha kuifanya Burnley kuondoka na pointi tatu kwenye mchezo wa Ligi Kuu England mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa Anfield na kuvunja rekodi ya Liverpool ya kutofungwa nyumbani tangu mwaka 2017.

Baaada ya mchezo huo, kocha wa klabu ya Liverpool Jurgen Klopp alisema kuwa licha ya kupoteza mchezo huo ila maamuzi ya wachezaji wake kwenye eneo la mwisho la wapinzani hayakuwa sahihi.

“Katika eneo la mwisho maamuzi yetu hayakuwa sahihi, hilo ndiyo tatizo, umepata mpira kwenye eneo sahihi badala ya kupiga shuti mchezaji anatoa pasi,” alisema Klopp na kuongeza:

“Tofauti ya mchezaji mzuri na mchezaji mzuri sana ni kwenye kufanya maamuzi uwanjani.”

Kwa matokeo haya dhidi ya Burnley yamevunja rekodi ya Liverpool ya kucheza michezo 68 ya Ligi Kuu kwenye dimba la Anfield na huku wakicheza michezo minne bila kufunga bao na mechi sita bila kupata ushindi.

Liverpool kwa sasa imeachwa nyuma kwa pointi sita na vinara wa Ligi hiyo Manchester United yenye pointi 40 na kushika nafasi ya nne kwenye msimamo wa Ligi Kuu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!