Wednesday , 29 March 2023
Home Kitengo Michezo Klopp awagwaya Leicester City
Michezo

Klopp awagwaya Leicester City

Spread the love

MENEJA wa klabu ya Liverpool, Jurgen Klopp ameonekana kuwahofia dhidi klabu ya Leicester City katika kuelekea kwenye mchezo wao wa ligi kuu nchini Uingereza utakaopigwa siku ya Jumamosi kwenye dimba la King Power. Anaripoti Kelvin Mwaipungu …. (endelea).

Klopp ambaye amechaguliwa kuwania tuzo ya kocha bora wa mwezi wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema kwa sasa Leicester wanaonekana kubadili aina yao ya mchezo, wanacheza vizuri na kwa kujiamini.

“Unaweza kuona kocha Claude Puel anafanya kazi nzuri, amebadilisha jinsi ya kucheza, ni mpira mzuri wanaocheza na kujiamini zaidi. Utakuwa mchezo mgumu kwetu,” amesema Klopp.

Liverpool ambayo mpaka sasa imeshinda michezo yao miwili iliyopita inapewa nafasi kubwa ya kutwaa taji la Ligi Kuu nchini humo kutokana kuwa na kikosi kizuri na kilichofanya vizuri katika msimu uliomalizika wa michuano ya klabu bingwa barani Ulaya licha ya kupoteza mchezo wao wa fainali dhidi ya Real Madrid.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

TANROADS wawataka watumishi wazingatie michezo kazini

Spread the love  WAKALA wa barabara Tanzania (TANROADS) imesema michezo inapaswa kuzingatiwa...

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

error: Content is protected !!