Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Klopp amwaga chozi, ubingwa wa Liverpool
Michezo

Klopp amwaga chozi, ubingwa wa Liverpool

Jurgen Klopp
Spread the love

KOCHA wa timu Liverpool Jurgen Klopp ameonesha hisia kali za furaha mara baada ya timu yake kutangaza ubingwa wa Ligi Kuu nchini England, baada ya Manchester City kufungwa na Chelsea kwa mabao 2-1. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Klopp ameonesha hisia hizo wakati akifanya mahojiano na kituo cha Sky Sport mara baada ya mchezo kati ya Chelsea na Manchester City kumalizika na kusema kuwa hakuwa na wazo kama atajisikia hivi.

“Tulilazimika kuwashawishi watu na hivi ndivyo tulivyofanya kwa pamoja, ni wakati mzuri, nimezidiwa kabisa sikujua ningejisikia hivi,” alisema Klopp.

Toka mara ya mwisho kuchukua ubingwa Jurgen Klopp anakuwa kocha wa tisa kukinoa kikosi hicho na kufanikiwa kumaliza ukata wa taji la Ligi Kuu.

Makocha hao waliopita tangu mwaka 1990 ni Graeme Souness (1991–1994), Roy Evans (1994-1998), Gerard Houllier (1998-2004), Rafael Benitez (2004-2010), Roy Hodgson (2010-2011), Kenny Dalglish (2011-2012), Brendan Rodgers (2012-2015) na Jurgen Klopp (2015-2020)

Liverpool iliwalazimu kusubili kwa muda wa miaka 30 kutwaa taji la Ligi Kuu nchini England toka walivyofanya mara ya mwisho 1990, chini ya kocha Kenny Danglish.

Ubingwa huu utakuwa wa 19, kwa klabu hiyo wakiwa nyuma ya Manchester United wenye mataji 20.

Baada ya taji hilo, Liverpool imeweka rekodi ya kutangaza ubingwa ikiwa imesalia michezo saba na kuvunja rekodi iliyowekwa na Manchester United walioiweka kwenye msimu wa 2000/01 walitangaza ubingwa wakiwa wamesalia na mechi tano.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!