SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeelezeka kuwa klabu yoyote ambayo inadaiwa na wachezaji haitoweza leseni na kushiriki michuano mbalimbali msimu ujao ikiwemo Ligi Kuu Tanzania Bara. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)
TFF imeleza hivyo kupitia taarifa yake iliyotolewa hii leo tarehe 27 Mei, 2021 mara baada ya kufunguliwa kwa maombi ya leseni kwa klabu zinazoshiriki Ligi Kuu, Ligio daraja la kwanza na Ligi daraja la pili katika msimu wa 2021/22.
Taarifa hiyo imeeleza kuwa zoezio la urudishwaji wa fomu wa maombi hayo litafungwa tarehe 15 Juni, 2021.
Aidha katika taarifa yao hiyo shirikisho hilo limeleza kuwa kuanzia msimu ujao wa mashindano 2021/21, klabu yoyote ambayo inadaiwa na mchezaji haitapatiwa leseni ya kushiriki Ligi katika ngazi zote.
“Kwa msimu ujao wa 2021/22 klabu yoyote itakayokuwa inadaiwa na mchezaji haitapatiwa leseni ya kushiriki Ligi.” ilieleza taarifa hiyo
Katika hatua nyingine taarifa hiyo ilitoa tahadhari ya timu zitakazoshiriki michuano ya CAF (Ligi ya mabingwa na kombe la Shirikisho) wakufunzi wao wanapaswa kuwa na leseni A na B ya shirikisho la mpira wa miguu barani Afrika.
“Klabu itakayoshiriki mashindano ya CAF, kocha mkuu ni lazima awe na leseni A ya CAF na kocha msaidizi ni lazima awe na leseni B ya CAF.” Ilimalizia taarifa hiyo
Leave a comment