Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Kiwanja cha ndege Manyara kujegwa
Habari za Siasa

Kiwanja cha ndege Manyara kujegwa

Spread the love

 

SERIKALI nchini Tanzania, inatarajia kuanza ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Mwada, mkoani Manyara. Anaripoti Nasra Bakari, DMC … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo Jumatatu tarehe 3 Mei 2021, na Mwita Waitara, Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, bungeni jijini Dodoma katika kipindi cha maswali na majibu.

Waitara alikuwa akijibu swali la Regina Qwaray, Mbunge wa Viti Maalum mkoani Manyara (CCM), aliyetaka kujua lini serikali itaweka mpango wa ujenzi wa kiwanja hicho mkoani Manyara.

Waitara amesema, serikali kupitia Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA), na kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara, wameainisha eneo la Mwada katika Halmashauri ya Wilaya ya Babati kwa ajili ya ujenzi wa kiwanja hicho.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!