KAMATI ya kuzuia na kupambana na dawa zisizo ruhusiwa michezoni ya kanda ya tano Afrika (RADO) imemfungia kiungo wa Yanga, Mohamed Issa ‘Banka’ kujihusisha na mchezo wa soka kwa kipindi cha miezi 14. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).
Adhabu hiyo ya Banka inaanza kuanzia tarehe 19 Deseemba, 2017 mpaka Febuari 8, 2019 kutokana na matumizi ya dawa za kulevya aina ya bangi.
Kiungo huyo ambaye alisajiriwa kutoka Mtibwa Sugar katika dirisha kubwa la usajiri alikutwa akitumia dawa hizo katika michuano ya CECAFA Chalenji, iliyofanyika Kenya mwaka jana, baada ya kumchukua vipimo vya mkojo na kwenda kufanyiwa uchunguzi kwenye maabara ya WADA iliyopo Doha, Qatar.
Ofisa habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Clifford Ndimbo amesema kuwa wakati wote huo Banka hataruhusiwa kufanya chochote kinachohusiana na michezo ikiwa ni kufanya mazoezi hadharani au kuonekana akishiriki shughuli za mpira wa miguu.
“Baada ya uchunguzi wa maabara na utetezi toka kwa mchezaji huyo, Kamati imemkuta na hatia na imemfungia kwa kipindi cha miezi 14 kuanzia Desemba 9, 2017 na adhabu inatarajiwa kumalizika Februari 8,2019,” alisema Ndimbo.
Hata hivyo baada ya kumkuta na hatia mchezaji huyo alikiri kosa na kuchagua kujitetea kwa njia ya maandishi baada ya kutakiwa kukubali au kukataa kosa na utetezi wake uliwasilishwa 1 Agosti, 2018 juu ya matumizi ya dawa hizo ambazo zinapigwa marufuku michezoni.
Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...
By Mwandishi WetuApril 16, 2024Spread the love IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...
By Mwandishi WetuApril 15, 2024Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na Klabu...
By Mwandishi WetuApril 15, 2024Spread the loveVIPENGELE vya mkataba wa kazi aliotia saini Kocha Mkuu wa...
By Masalu ErastoApril 15, 2024
Leave a comment