Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Kitillya, wenzake: Faini Bil 1.5 au jela miezi sita
Habari Mchanganyiko

Kitillya, wenzake: Faini Bil 1.5 au jela miezi sita

Spread the love

MAHAKAMA Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu uchumi nchini Tanzania, imemhukumu Harry Kitillya, aliyekuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) na wenzake kwenda jela miezi sita au kulipa faini ya Shilingi 1.5 Bilioni. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam…(endelea).

Washtakiwa wengine kwenye shauri hilo ni pamoja na Shose Sinare, Sioi Solomon, Bedason Shallanda na Alfred Misana. Kwa pamoja washtakiwa hao walikiri makosa yao.

Shose ni alikuwa Ofisa wa Kitengo cha Uwekezaji kwenye benki ya Stanbick pia alikuwa Miss Tanzania 1996, Solomon alikuwa Mwanasheria wa Benki hiyo.

Shallanda alikuwa Ofisa wa Sera kwenye Wizara ya Fedha za uchumi, Misana akiwa Kamishana msaidizi Kitengo cha Madeni kwenye idara ya Sera wizarani hapo.

Washtakiwa hao walikubali kulipa faini hiyo ambapo kila mmoja alitakiwa kulipa Sh. 1 Mil kutoka na kesi ya uhujumu uchumi inawakabili. Hukumu hiyo imetolewa jana Jumanne tarehe 25 Agosti 2020 na jaji wa mahakama hiyo, Immaculate Banzi.

Washtakiwa hao walifutiwa mashtaka 57 na kubaki shitaka moja la kuisababishia serikali hasara kiasi cha Dola za Marekani milioni 600. Kesi hiyo ilianza kupitiwa jana saa 11 na kuisha saa 2 usiku.

Washtakiwa wanadaiwa kutenda kosa hilo kati ya Machi 2013 na Septemba 2015, wakati wa mchakato wa mkopo wa Dola za Marekani milioni 550 kwa Serikali ya Tanzania kutoka Benki ya Standard ya Uingereza.

Aidha, wanadaiwa kula njama za kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu ili kujinufaisha wenyewe na washirika wao. Kwenye kesi hiyo, mawakili wa washtakiwa walikuwa Alex Mgongolwa na Jeremiah Mtobesya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!