Saturday , 2 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Kitachofanywa na JPM siku tano za ziara yake Dodoma
Habari za Siasa

Kitachofanywa na JPM siku tano za ziara yake Dodoma

Jiji la Dodoma
Spread the love

RAIS John Magufuli anatarajiwa kufanya ziara ya siku tano jijini Dodoma, kuanzia tarehe 21 – 25 Novemba 2019. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari, leo tarehe 20 Novemba 2019, Dk. Binilith Mahenge, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma amesema, Rais Magufuli atatembelea miradi inayotekelezwa kwenye jiji hilo.

Amesema, miongoni mwa shughuli atazofanya Rais Magufuli ni pamoja na kuwa mgeni rasmi katika mahafali ya 10 katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), siku ya Alhamisi tarehe 21 Novemba mwaka huu.

Dk. Mahenge amesema, Ijumaa ya tarehe 22 Novemba 2019, atatembelea na kuweka jiwe la msingi kwenye mradi wa Hospitali ya Uhuru Wilayani Chamwino, Ujenzi wa Nyumba 118 za polisi katika maeneo ya FFU Nzuguni na Medel East.

Pia ataweka jiwe la msingi katika ujenzi wa Stendi Kuu ya mabasi iliyopo Nzuguni na Soko Kuu linalojengwa katika eneo la Nzuguni.

Amesema, tarehe 25 Novemba 2019, Rais Magufuli ataweka jiwe la msingi kwenye mradi wa ujenzi wa Makao Makuu ya Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) – Kikombo, ujenzi wa Ofisi ya Makao Makuu ya Idara ya Uhamiaji na Ujenzi wa Jengo la Makandarasi eneo la National Capital City.

Na kwamba, maandalizi ya ziara hiyo yamekamilika, ambapo ametoa wito kwa wananchi wote kujitokeza ili kumsikiliza Rais Magufuli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia kuzindua programu ya nishati safi ya kupikia kwa wanawake Afrika

Spread the loveRais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuzindua programu ya...

Habari za Siasa

AG aiagiza kamati ya maadili kuwashughulikia mawakili wanaokiuka maadili

Spread the loveMWANASHERIA Mkuu wa Serikali (AG), Dk. Eliezer Feleshi, ameagiza Kamati...

Habari za Siasa

Jaji avunja ukimya sakata la Mpoki kusimamishwa uwakili

Spread the loveJAJI Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Juma, amekitaka Chama cha...

Habari za Siasa

Sheikh Ponda ataka mwarobaini changamoto uchaguzi 2020

Spread the loveKATIBU Mkuu wa Shura ya Maimamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa...

error: Content is protected !!