Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kiswahili kutumika usaili kazi Serikalini
Habari za Siasa

Kiswahili kutumika usaili kazi Serikalini

Waziri wa Fedha na Mpango wa Tanzania, Dk. Mwigulu Nchemba
Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania imetangaza kusudio la kutumia Kiswahili katika kufanya usaili wa watumishi umma. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea)

Mwigulu ametangaza mapendekezo hayo leo Jumanne tarehe 14 Juni 2022 bungeni jijini Dodoma akiwasilisha bajeti kuu ya Serikali kwa mwaka 2022/23.

Waziri huyo amesema lugha ya kiswahili “ndio lugha ya Taifa, ndio lugha ya ofisini, ndio lugha ya pili kwa watoto wa vijijini na lugha ya kwanza kwa watoto waliowengi wa sasa, ndio lugha ya msingi, ni lugha ya Bunge, na nikiwa Waziri wa Katiba na Sheria nilileta mapendekezo kuifanya kuwa lugha ya Mahakama na lugha ya hukumu.”

“Hii ndiyo lugha yetu, kwa nini usaili wa mtoto wa kitanzania anapotafuta kazi unafanyika kwa lugha ya Kingereza?” amehoji Dk. Nchemba na kuongeza;

“Yaani afisa kilimo, afisa mifugo, mtumishi wa Serikali anakazi ya kuhudumia watanzania tunapima akili zake kwa kupima kingereza chake kwa ajili ya nini? Ameendelea kuhoji.

“Napendekeza saili zote zifanyike kwa Kiswahili, na kumbi zote za mikutano na ofisi za Serikali ziwe na vifaa vya kutafsiria lugha za kigeni na watafsiri ili tuweze kuienzi lugha yetu ya Taifa,” amesema.

Amesema Kiswahili ni lugha ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) “ambapo tumeipeleka wenyewe, ikiwa ni pamoja na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na Umoja wa Afrika (AU).
Vilevile, amesema UNESCO wameitambua na watakuwa wanaiadhimisha tarehe 7 Julai kila mwaka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!