Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari Kisinda, Ntibazonkiza wafunga dirisha la usajili Tanzania
HabariMichezo

Kisinda, Ntibazonkiza wafunga dirisha la usajili Tanzania

Spread the love

 

WACHEZAJI wa kimataifa Tuisila Kisinda pamoja na nyota kutoka Burundi Saido Ntibanzokiza wameng’ara dakika za mwisho wakati wa kufungwa kwa dirisha la usajili wa Ligi Kuu Taanzania Bara kwa msimu wa 2022/23. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Usajili huo wa dirisha kubwa uliodumu katika kipindi cha miezi miwili ulifungwa rasmi jana tarehe 31 Agosti 2022, majira ya saa 5:59 usiku.

Muda mchache kabla dirisha hilo kufungwa, Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara walifanikiwa kuinasa kwa mara nyingine, Saini ya nyota wao wa zamani raia wa Kidemokrasia ya Congo, Tuisila Kisinda akitokea nchini Morocco kwenye klabu ya RS Berkane ambao ni mabingwa watetezi wa michuano ya kombe la Shirikisho Barani Afrika.

Ujio wa Kisinda ndani ya Yanga, unamfanya kuwa mchezaji wa 14 kati ya 12 wanaohitajika kwa mujibu wa kanuni, huku kitendawili kikubwa kikiwa wachezaji gani wataondolewa ndani ya kikosi hiiko ili kutimiza idadi kamili inayoyotakiwa.

Kwa upande wa klabu ya Geita Gold ambao nao wanakibarua msimu huu cha kuiwakilisha nchi kwenye michuano ya kombe la Shirikisho Barani Afrika, hawakuwa nyuma kwenye dakika hizo za mwisho za usajili na kufanikiwa kumtangaza aliyekuwa mchezaji wa zamani wa klabu ya Yanga, Saido Ntibanzokiza.

Taarifa rasmi iliyotolewa na klabu hiyo, imeeleza kuwa mchezaji huyo raia wa Burundi amefanikiwa kuingia mkataba wa mwaka mmoja ambapo atakwenda kuongeza nguvu kwenye safu ya ushambuliaji ya klabu hiyo.

Ligi hiyo ambayo kwa sasa imesimama, itarejea tena tarehe 5 mwaka huu, mara baada ya kupisha kalenda ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Afrika (CAF), katika kutafuta tiketi ya kufuzu kwa faib]nali za michuano ya kombe la Mataifa Afrika kwa wachezaji wa ndani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!