SERIKALI ya Ufaransa imetangaza kuwaachisha kazi wahudumu wa afya 3,000 waliogoma kuchanjwa chanjo ya Corona licha ya nchi hiyo kupitisha sheria ya lazima kwa wahudumu wa sekta hiyo kuchanjwa. Anaripoti Helena Mkonyi TUDARCo kwa msaada wa vyombo vya habari vya kimataifa … (endelea).
Pia mmoja wa watatibu hao Thierry Paysant ametangaza mgomo wa njaa yaani kutokula hadi hapo Serikali itakapowarejesha kazini.
Paysant ambaye alikuwa mhudumu wa kitengo cha udhibiti moto katika hospitali ya Nice nchini humo, aliandamana mitaani huku akiwa na bango lililoandikwa ‘mgomo wa njaa’ na kusisitiza kuwa mbali na hatua hiyo watachukua hatua zaidi kuishinikiza serikali.
Paysant amesema hakuwa na nia ya kwenda kinyume na matakwa ya taratibu za chanjo lakini kitendo cha serikali kuwatimua wafanyakazi wenzie kisha kushindwa kuchanja kabla ya tarehe ya mwisho kuchanja ndicho kilichomkera.
“Nina huzuni ambayo haielezeki kwa sababu chanjo yenye imeletwa kwa vurugu na kuanza kutulazimisha wakati hii inapaswa kuwa hiyari,” amesema.
Aidha, Waziri wa Afya nchini humo, Olivier Veran ametangaza kuwa tarehe ya mwisho wa kuchanja ilikuwa jana tarehe 15 Septemba, 2021 ndio maana leo Serikali imechukua hatua ya kuwatimua wafanyakazi hao.
Amesema Serikali imeamua kuchukua uamuzi huo ili kudhibiti maambukizi ya virusi vya Corona nchini humo.
Kwa mujibu wa mtandao wa takwimu za kila muda duiani ‘Worldometer’, hadi kufikia tarehe 16 Septemba Ufaransa ilikuwa na maambukizi ya Corona milioni 6.9 huku kukiwa na vifo 115,829.
Leave a comment