Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Kisa corona: ATCL yasitisha safari Tanzania-India
Habari Mchanganyiko

Kisa corona: ATCL yasitisha safari Tanzania-India

Ndege ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL)
Spread the love

 

JANGA la ungonjwa unaosababishwa na virusi vya corona (COVID-19), unaoendelea kushika kasi nchini India, umesababisha Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL), kusitisha safari zake kati ya Dar es Salaam-Tanzania kwenda nchini humo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Hadi leo asubuhi Jumatano, tarehe 5 Mei 2021, maambukizi ya corona nchini India, yamefikia milioni 20.66, ikiwa nchi ya pili kwa maambukizi dunia, ikitanguliwa na Marekani yenye maambukizi milioni 33.27.

Kati ya maambukizi milioni 20.66 ya India, waliofariki dunia wakiwa 226,188 na waliopona ugonjwa huo wakiwa milioni 16.95.

Kutokana na janga hilo, jana Jumanne, tarehe 4 Mei 2021, Mkurugenzi Mtendaji wa ATCL, Mhandisi Ladislaus Matindi alitangaza kusitishwa kwa safari za ndege kwenda India.

Alisema, abiria wote wenye tiketi za ATCL, wanashauriwa kuwasiliana na ofisi za ATCL au mawakala wao kwa taratibu za kubadilisha tiketi ili zitumike pindi safari zitakaporejeshwa tena bila gharama yoyote.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mchina wa SGR aburuzwa kortini kwa kumjeruhi Mtanzania, TRC waja juu

Spread the love  RAIA wa China, Zheng Yuan Feng, amefikishwa mahakamani kwa...

Habari Mchanganyiko

Watendaji Kata, Mitaa watakaoshindwa kusimamia usafi kukiona

Spread the love  WATENDAJI wa kata, mitaa na vitongoji na maofisa afya...

Habari Mchanganyiko

Mtia nia urais TLS kukata rufaa kupinga kuenguliwa

Spread the love  MTIA nia ya kugombea Urais wa Chama cha Mawakili...

Habari Mchanganyiko

NBC yazindua kampeni ya mkeka wa ushindi na ATM zake

Spread the loveBENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imetangaza uzinduzi wa kampeni...

error: Content is protected !!