Thursday , 30 March 2023
Home Kitengo Maisha Afya Kirusi kipya cha Corona chatikisa, chadaiwa kuishinda nguvu chanjo
AfyaKimataifa

Kirusi kipya cha Corona chatikisa, chadaiwa kuishinda nguvu chanjo

Spread the love

 

KIRUSI kipya cha Corona kilichopewa jina la ‘Mu’ au  B.1.621 kimeanza kutikisa nchi kadhaa za Bara la Amerika kusini na Ulaya huku kikidaiwa kuwa kinaweza kukwepa chanjo ya Corona. Anaripoti mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

WHO ilisema kirusi hicho kina mabadiliko yanayoonesha hatari ya kuishinda nguvu ya chanjo na kwamba utafiti zaidi unahitajika kukielewa.

Hayo yamebainishwa tarehe 30 Agosti mwaka huu na Shirika la Afya Duniani (WHO) kupitia jarida lake baada ya Shirika hilo kukingiza kirusi hicho katika orodha ya virusi hatari vya Corona.

Kirusi hicho ambacho kilianza kugunduliwa huko nchini Colombia, hadi sasa kimeathiri nchi 389 kati bara la Amerika Kusini, Kaskazini na Ulaya.

Kwa mujibu wa Ofisa wa afya nchini Colombia, Marcela Mercado  amesema kirusi MU ndicho kinachosambaa zaidi nchini humo na kinahusika na wimbi baya zaidi la janga la corona.

Mercado ameiambia redio moja nchini humo kwamba kirusi cha “Mu” kinahusika na wimbi kali la tatu la maambukizi kati ya April na Juni mwaka huu.

Nchi hiyo ambayo imekuwa ikirekodi vifo 700 kila siku vitokanavyo na Corona, karibu theluthi mbili ya vipimo vilivyofanywa kutoka kwa watu waliofariki vilionesha waliambukizwa kirusi cha Mu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Nyumba ya babu yake Makamu wa Rais wa Marekani yatafutwa Zambia

Spread the love  KAMALA Harris, makamu wa rais wa Marekani, amepanga kutembelea...

Kimataifa

Benki ya Uswizi mbioni kuziwekea vikwazo akaunti za siri za Wachina

Spread the love  WAKATI Serikali na Benki ya Uswizi ikichukua hatua kali...

Kimataifa

Netanyau asitisha mipango yenye utata marekebisho mfumo wa sheria

Spread the love  WAZIRI Mkuu wa nchini Israel, Benjamin Netanyahu amesema atachelewesha...

Kimataifa

Raila ahutubia waandamanaji, mabomu yarindima

Spread the loveMSAFARA wa kiongozi wa Azimio la Umoja-One Kenya, Raila Odinga...

error: Content is protected !!