Aliyekuwa mlinda mlango wa klabu ya Yanga Ramadhan Kabwili, rasmi amejiunga na klabu ya soka ya Rayon Sport ya nchini Rwanda kama mchezaji huru mara baada ya kumalizika kwa mkataba na klabu yake ya zamani ya Yanga. Anaripoti Damas Ndelema………(endelea)
Mchezaji huyo amesaini mkataba wa mwaka mmoja kuweza kuitumikia klabu hiyo, inayoshiriki Ligi Kuu nchini Rwanda ambyao wanapambana kutengeneza timu yao ili kurejesha ufalme wao katika soka la nchini humo baada ya msimu uliopita kushika nafasi ya nne kwenye Ligi Kuu nchini humo.
Kipa huyo alieibukia katika michuano ya Afcon 2017 akionesha kiwango bora akiwa na timu ya Taifa ya vijana kisha kujiunga na timu ya Yanga ambpo alipewa kandarasi ya miaka mitano.
Kabwili amesajiliwa kwenye klabu bhiyo kwa mapendekezo ya kocha wa makipa wa timu hiyo, Vladimir Niyonkuru raia wa Burundi ambae pia aliwahi kufanya nae kazi wakiwa wote kwenye klabu ya Yanga, chini ya kocha Mwinyi Zahera raia wa Congo.
Mlinda mlango huyop alithibitisha rasmi kijiunga na miamba hiyo ya nchini Rwanda, kupitia kurasa yake inayopatikana kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram na kuandika kuwa ni muda wa kufungua ukurasa mpya.
Leave a comment