Tuesday , 23 April 2024
Home Kitengo Michezo Kiongozi Yanga amkataa Ajibu
MichezoTangulizi

Kiongozi Yanga amkataa Ajibu

Ibrahim Ajibu, mshambuliaji wa Yanga
Spread the love

 

Mara baada ya kuwepo kwa fununu nyingi ya mshambuliaji wa klabu ya Simba Ibrahim Ajibu kutaka kusaini Yanga, Arafati Haji ambaye ni mmoja ya mjumbe wa kamati tendaji ya klabu hiyo amefunguka kuwa mchezaji huyo hawezi kusaini Yanga. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Maneno ya kiongozi huyo yamekuja kufuatia andiko lililowekwa na mmoja ya mchambuzi wa maswala ya mpira kwenye mtandao wa Twiiter na kuonesha faida ambayo Yanga watapata ndani ya Uwanja kama wakimrejesha mchezaji huyo.

https://twitter.com/privaldinho/status/1399801605260722176

Katika kujibu taarifa hiyo kiongozi huyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa kamati ya Fedha ndani ya klabu hiyo aliona kama mchambuzi huyo anampigia debe ajibu kurejea Yanga na kumwambia kuwa wamtafutie timu nyingine na Yanga aliyokuwepo yeye haiwezi kumsajili.

Ajibu kwa sasa anamaliza mkataba wake ndani ya Simba mara baada ya msimu huu kukamilika na anahusishwa na tetesi nyingi za za kurejea kwenye klabu yake ya awali ya Yanga ambayo aliitumikia kwa miaka miwili.

Arafat Haji, Mjumbe wa kamati ya utendaji Yanga

Toka amerejea ndani ya kikosi cha Simba mchezaji huyo ameonekana kutopata nafasi ya kucheza mara kwa mara kutokana na kikosi hiko kusheheni wachezaji hodari katika kila idara.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

Michezo

Ujanja ni kubeti na Meridianbet

Spread the love  JUMAPILI ya leo imekaa kihela hela sana ndani ya...

error: Content is protected !!