Aliyekuwa Mwenyekiti wa klabu ya Simba Swedy Nkwabi pamoja na Philemon Ntahilaija wamejitokeza kwenye makao Makuu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kumchukulia fomu Wallace Karia kwenye uchaguzi Mkuu wa Tff utakaofanyika tarehe 7 Agosti, 2021. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)
Uchaguzi huo mwaka huu utafanyika mkoani Tanga ambao wadau hao wawili walimchukulia fomu Karia ambaye anatetea kiti chake cha Urais mara baada ya muda wa awali wa miaka minne kumalizika.
Wadau hao walifika kwenye ofisi hizo za Tff majira ya saa 8 mchana huku wakiwa na risiti za malipo ya benki kama gharama za fomu ambapo ilikuwa shilingi 500,000.
Mara baada ya kuchukua fomu hiyo kwenye ofisi za Tff Nkwabi alifunguka sababu za wao kumchukulia fomu Karia ili kutetea kiti chake na kusema kuwa wanataka aendeleze yale mazuri aliyofanya katika kipindi cha miaka minne.
“Mimi nimekuja kuchukua fomu kwa niaba ya Rais Wallace Karia, kumuomba kwamba atetee nafasi yake ya urais, aendeleze mazuri alishowahi kuyafanya katika kipindi hiki kinachofuata.” Alisema Nkwabi
Aidha Nkwabi aliongezea kusema kuwa kwa kiasi kikubwa Karia amefanikiwa katika uongozi wake hasa kwenye timu ya Taifa (Taifa Stars), sola la wanawake pamoja na mpira wa ufukweni (Beach soccer)
“Kwa kiasi kikubwa amefanikiwa sana, na nyie ni mashahidi mmeona mpira wa wanawake ulipofikia, beach Soccer na timu yetu ya taifa imeshikili mashindano yote muhimu na kiasi imefanya vizuri.” Alinena Nkwabi
Leave a comment