Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kinana awapa maagizo wabunge, madiwani
Habari za Siasa

Kinana awapa maagizo wabunge, madiwani

Abdulrahman Kinana, Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara
Spread the love

 

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Abdulrahman Kinana amewataka madiwani na wabunge kukataa kupitisha miswada ya sheria yenye kukandamiza haki na kuminya fursa ya wananchi wanyonge kujiendeleza kiuchumi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Korogwe … (endelea).

Pia, amesema sasa ni wakati muafaka kulitazama vyema kundi la wajasiriamali wadogo wakiwemo mamalishe na bodaboda ili wawekewe mazingira mazuri ya kunufaika na juhudi zao.

Kinana ameyasema hayo leo Jumatatu, tarehe 25 Aprili 2022 mjini Korogwe, Mkoa wa Tanga wakati akizungumza na wana CCM katika ukumbi wa Lembeni, akiwa katika ziara ya kukagua uhai wa Chama na kujitambulisha kwa wanachama.

“Madiwani nyinyi ndio mnaosimamia sheria za Halmashauri, mkiona sheria hazina uhusiano na wananchi kataeni. Mkiletewa sheria pelekeni kwa wananchi waulizeni, rahisisheni maisha ya watu muwasidie wakue,” amesema na kuongeza:

“Wabunge wa Bungee la Jamhuri ya Muungano…sheria ikija bungeni waambieni (serikali) kwa sasa hatuipitishi mpaka tukashauriane na wananchi,” alisema.

Kinana ameanza ziara mikoa ya Pwani, Tanga, Kilimanjaro na Arusha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Mwakyembe : Zanzibar waliongoza kutaka Serikali 2 za muungano

Spread the love  MWANASIASA mkongwe nchini, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema mjadala wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

error: Content is protected !!