Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kinachoendelea kesi ya kina Mbowe, RPC Kingai anatoa ushahidi
Habari za SiasaTangulizi

Kinachoendelea kesi ya kina Mbowe, RPC Kingai anatoa ushahidi

Spread the love

 

KESI ya uhujumu uchumi yenye mashtaka ya ugaidi inayomkabili kiongozi wa chaa kikuu cha upinzani nchini Tanzania cha Chadema, Freeman Mbowe na wenzake watatu, inaanza kusikilizwa mfululizo kuanzia leo Jumatano, tarehe 15 Septemba 2021. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea). 

Mbali na Mbowe wengine; ni Halfani Bwire Hassan, Adam Kasekwa na Mohammed Abdillah Lingwenya.

Jaji anayesikiliza kesi hiyo Mustapha Siyai ameingia ndani ya chumba cha Mahakama na kuiita kesi hiyo.

Wakili wa serikali mwandamizi, Robert Kidando, ameieleza Mahakama kuwa wamekuja mahakamani kusikiliza shauri na wamewaleta mashahidi wawili.

Miongoni mwa mashahidi waliopo tayari mahakamani kutoa ushahidi ni, Kamanda wa Polisi wa Kinondoni (RPC), Ramadhan Kingai.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI TV, MwanaHALISI Online na mitandao yetu ya kijamii kwa habari na taarifa mbalimbali.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!