Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kina Mdee waibwaga Chadema mahakamani
Habari za SiasaTangulizi

Kina Mdee waibwaga Chadema mahakamani

Spread the love

 

WABUNGE Viti Maalum 19 wakiongozwa na Halima Mdee, wamekibwaga Chama cha Chadema mahakamani baada ya Mahakama Kuu, Masjala Kuu ya Dar es Salaam, kukubali ombi lao la kufungua kesi ya kupinga mchakato uliotumiwa na chama hicho kuwavua uanachama. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Uamuzi huo umetolewa leo Ijumaa tarehe 8 Julai, 2022, na Jaji Mustafa Ismail, kuhusu maombi hayo yaliyofunguliwa na kina mdee dhidi ya Chadema, Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG).

Jaji Ismail amewataka kina Mdee wafungue kesi hiyo ndani ya siku 14 kuanzia leo.

Katika maombi hayo, Mdee na wenzake 18 waliiomba mahakama ifanye mapitio ya kimahakama dhidi ya mchakato ambao Chadema ulitumia kuwavua uanachama, wakidai haukuwa halali kwani haukufuata sheria kwa kuwa hawakupewa nafasi ya kusikilizwa na kugubikwa na upendeleo.

Hata hivyo, Chadema kupitia mawakili wake, wakiongozwa na Wakili Peter Kibatala, waliiomba mahakama ikatae ombi la kina Mdee kwa kuwa hoja zao hazina mashiko wakidai walipewa nafasi ya kusikilizwa.

Wakili wa Chadema, wakiongozwa na Peter Kibatala (katikati) wakiwa mahakamani

Mbali na Mdee, baadhi ya wabunge wengine ni Jesca Kishoa, Ester bulaya, Esther Matiko, Hawa Mwaifunga, Grace Tendega, Angesta Lambart, Ceciia Pareso, Asia Mwadin Mohamed, Felister Njau, Naghenjwa Kaboyoka, Sophia Mwakagenda, Kunti Majala, Stella Siyao, Salome Makamba, Anatropia Theonest na Conchesta Lwamlaza.

Wabunge hao walivuliwa uanachama wa Chadema tarehe 27 Novemba 2020, siku tatu baada ya kuapishwa na Spika Job Ndugai, kuwa wabunge viti maalumu kupitia chama hicho.

Mdee na wenzake walituhumiwa kwa makosa ya kusaliti msimamo wa Chadema wa kutopeleka wawakilishi wake bungeni, wakipinga matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 28 Oktoba 2020, kwa madai kwamba haukuwa huru na wa haki.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!