Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko KIMENUKA! Polisi watoa tamko trafki aliyenaswa tuhuma za rushwa
Habari Mchanganyiko

KIMENUKA! Polisi watoa tamko trafki aliyenaswa tuhuma za rushwa

Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania, David Misime
Spread the love

 

JESHI la Polisi nchini limesema tayari uchunguzi umeanza dhidi ya picha zilizosambaa katika mitandao ya kijamii huku zikimuonesha askari wa usalama barabarani (trafki) akiwa ameshika fedha mkononi.

Picha nyingine zilionesha fedha zikiwa ndani ya gari kwenye kiti huku picha hizo ziiambatana na ujumbe unaosema “ askari akamatwa akiwa na pesa za rushwa”. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo tarehe 20 Januari, 2022 na Msemaji wa Jeshi la Polisi, SACP- David Misime imesema picha hizo zilivyoanza kusambaa hatua zilianza kuchukuliwa kwa kushirikiana na wadau wengine.

Pia taarifa hiyo imeeleza kuwa hakuna aliyepo juu ya sheria hivyo hatua kali na stahiki kwa mujibu wa sheria, kanuni, taratibu na ushahidi utakaopatikana zitachukuliwa.

Aidha, taarifa za awali zinadai kuwa Askari huyo wa usalama barabarani wa Mkoa wa Iringa, anadaiwa kukamatwa na fedha anazodaiwa kuzikusanya kama zao la rushwa kutoka kwa madereva na wamiliki wa magari Januari 18, 2022.

Picha za tukio hilo zilionyesha ndani ya gari kukiwa na noti za Sh1,000, Sh2,000, Sh5,000 na Sh10,000 zilizokunjwa na nyingine askari mmoja akiwa amezishika baada ya kuzipanga.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!