
KIMBUNGA cha Maria kimekivuruga kisiwa cha Puerto Rico nchini Marekani na kusababisha umeme kukatika katika eneo lote katika kisiwa hicho, anaandika Mwandishi wetu.
Huu ni mfululizo wa Vimbunga katika nchi hiyo kubwa na yenye nguvu kiuchumi duniani.
Kimbunga Maria kimekata umeme katika kisiwa chote cha Puerto Rico, chenye watu milioni 3.5.
Abner Gómez, ambaye ni mkuu wa utoaji huduma za dharura amesema kuwa watu wote wanaotumia umeme wamekosa huduma hiyo.
Kituo cha vimbunga cha Marekani kinasema kuwa mafuriko makubwa yanaikumba nchi hyo.
Kwa sasa Kimbunga Maria kwa sasa kinaondoka eneo hilo na kumepunguza nguvu zake hadi kiwango cha pili.
Baada ya kimbunga Maria kuipiga Puerto Rico, gavana ameamrisha watu kusalia nyumbani kuanzia saa 12 jioni hadi asubuhi.
Hii ni hatua ya kwanza ya kuwazuia watu kusalia nyumbani ili kuwaepusha na ajali kutokana na nyaya za umeme zilizoanguka.
More Stories
Milioni 91 wapona corona duniani
Papa Francis atembelea Iraq
Kesi mauaji ya Jamal Khashoggi yaanza tena