Sunday , 3 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Kilichozungumzwa kati ya Magufuli na Rais mteule wa Burundi
Habari za Siasa

Kilichozungumzwa kati ya Magufuli na Rais mteule wa Burundi

Evariste Ndayishimiye, Rais wa Burundi
Spread the love

RAIS wa Tanzania, John Pombe Magufuli amezungumza kwa njia ya simu na Rais Mteule wa Jamhuri ya Burundi, Evariste Ndayishimiye na kumpongeza kwa uamuzi wa Mahakama ya Katiba nchini Burundi iliyoagiza Rais Mteule aapishwe haraka. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Katika mazungumzo hayo, Rais Magufuli amemtakia heri, Rais Mteule Ndayishimiye kuelekea kuapishwa kwake kuwa Rais wa Jamhuri ya Burundi kutakakofanyika hivi karibuni.

Taarifa iliyotolewa leo Jumamosi tarehe 13 Juni 2020 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa imesema Rais Magufuli amemhakikishia Rais Mteule Ndayishimiye kuwa Tanzania itaendeleza na kukuza zaidi uhusiano na ushirikiano wake wa karibu na Burundi kwa kuwa nchi hizo ni majirani, marafiki na ndugu wa kihistoria.

Rais John Magufuli

Rais Magufuli amerudia kumpa pole kwa msiba wa kuondokewa na Rais wa nchi hiyo, Pierre Nkurunziza aliyefariki dunia tarehe 09 Juni, 2020 na amemueleza kuwa yeye na Watanzania wote wanaungana na Warundi katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo.

Amemuomba kufikisha salamu zake za rambirambi kwa Warundi wote na kuwasihi waendelee kuwa watulivu na wastahimilivu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Biteko aagiza wakurugenzi TANESCO kukemea rushwa kwenye maeneo yao

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Uongozi wa Samia kuendelea hadi 2030

Spread the loveKWETU sisi tuliowahi kusoma sekondari, iwe O levo au A...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Bado askari wastaafu wanaonewa

Spread the loveRAIS wangu Samia Suluhu Hassan tunaendelea kumshukuru Mungu kwamba wote...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Tunastawisha ufisadi na kuchukia matunda yake

Spread the loveBUNGE la Jamhuri linaloendelea mjini Dodoma, kwa wiki nzima limetawaliwa...

error: Content is protected !!