Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Kikwete: Kwa heri kaka yangu Bakari Mwapachu
Habari Mchanganyiko

Kikwete: Kwa heri kaka yangu Bakari Mwapachu

Spread the love

 

JAKAYA Mrisho Kikwete, Rais mstaafu wa awamu ya nne wa Tanzania, amesema Taifa litamkumbuka mwanasiasa mkongwe nchini humo, Bakari Harith Mwapachu (81), kwa mchango wake alioutoa enzi za uhai wake. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea)

Mwapachu aliyewahi kuwa waziri wa katiba na sheria, alifariki dunia alfajiri ya jana Ijumaa tarehe 12 Februari 2021, katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, jijini Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu.

Mwapachu aliyehudumu tangu serikali ya awamu ya kwanza hadi ya nne, amewahi kuwa mbunge wa Tanga Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), kati ya mwaka 2000-2010, mwili wake utazikwa leo Jumamosi jijini Tanga.

Kikwete akiwa madarakani kati ya mwaka 2005 hadi 2015, alifanya kazi na Mwapachu ambapo, katika ukurasa wake wa Twitter, Kikwete amezungumzia kifo cha mwanasiasa huyo, aliyezaliwa tarehe 25 Julai 1939.

Bakari Harith Mwapachu

Akiambatanisha picha ya Mwapachu aliyopigwa enza za uhai wake katika moja ya matukio walipokutana, Kikwete ameandika “Innalillah Wainna Ilaihi Rajiun. Kwa heri kaka yangu Mhe. Bakari Mwapachu.”

“Daima tutakukumbuka kwa moyo wako wa upendo, huruma na ucheshi. Vilevile utakumbukwa kwa mema mengi uliyoifanyia nchi yetu na watu wake na kwa mchango muhimu uliotoa kwa ujenzi wa taifa letu,” amesema Kikwete

Rais huyo mstaafu amesema “poleni wanafamilia na ndugu zangu wote kwa msiba mkubwa uliowakuta. Ni msiba wetu sote. Tunawaombea kwa mola awape moyo wa subira katika kipindi hiki kigumu cha majonzi na kuomboleza.”

“Tuendelee kuomba kwa Mola amsamehe makosa na amjaalie pepo marehemu wetu. Ameen.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mchina wa SGR aburuzwa kortini kwa kumjeruhi Mtanzania, TRC waja juu

Spread the love  RAIA wa China, Zheng Yuan Feng, amefikishwa mahakamani kwa...

Habari Mchanganyiko

Watendaji Kata, Mitaa watakaoshindwa kusimamia usafi kukiona

Spread the love  WATENDAJI wa kata, mitaa na vitongoji na maofisa afya...

Habari Mchanganyiko

Mtia nia urais TLS kukata rufaa kupinga kuenguliwa

Spread the love  MTIA nia ya kugombea Urais wa Chama cha Mawakili...

Habari Mchanganyiko

NBC yazindua kampeni ya mkeka wa ushindi na ATM zake

Spread the loveBENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imetangaza uzinduzi wa kampeni...

error: Content is protected !!