Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Kikwete: Kwa heri kaka yangu Bakari Mwapachu
Habari Mchanganyiko

Kikwete: Kwa heri kaka yangu Bakari Mwapachu

Spread the love

 

JAKAYA Mrisho Kikwete, Rais mstaafu wa awamu ya nne wa Tanzania, amesema Taifa litamkumbuka mwanasiasa mkongwe nchini humo, Bakari Harith Mwapachu (81), kwa mchango wake alioutoa enzi za uhai wake. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea)

Mwapachu aliyewahi kuwa waziri wa katiba na sheria, alifariki dunia alfajiri ya jana Ijumaa tarehe 12 Februari 2021, katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, jijini Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu.

Mwapachu aliyehudumu tangu serikali ya awamu ya kwanza hadi ya nne, amewahi kuwa mbunge wa Tanga Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), kati ya mwaka 2000-2010, mwili wake utazikwa leo Jumamosi jijini Tanga.

Kikwete akiwa madarakani kati ya mwaka 2005 hadi 2015, alifanya kazi na Mwapachu ambapo, katika ukurasa wake wa Twitter, Kikwete amezungumzia kifo cha mwanasiasa huyo, aliyezaliwa tarehe 25 Julai 1939.

Bakari Harith Mwapachu

Akiambatanisha picha ya Mwapachu aliyopigwa enza za uhai wake katika moja ya matukio walipokutana, Kikwete ameandika “Innalillah Wainna Ilaihi Rajiun. Kwa heri kaka yangu Mhe. Bakari Mwapachu.”

“Daima tutakukumbuka kwa moyo wako wa upendo, huruma na ucheshi. Vilevile utakumbukwa kwa mema mengi uliyoifanyia nchi yetu na watu wake na kwa mchango muhimu uliotoa kwa ujenzi wa taifa letu,” amesema Kikwete

Rais huyo mstaafu amesema “poleni wanafamilia na ndugu zangu wote kwa msiba mkubwa uliowakuta. Ni msiba wetu sote. Tunawaombea kwa mola awape moyo wa subira katika kipindi hiki kigumu cha majonzi na kuomboleza.”

“Tuendelee kuomba kwa Mola amsamehe makosa na amjaalie pepo marehemu wetu. Ameen.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!