Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kikwete: JPM amewazima midomo wapinzani ajenda ya rushwa
Habari za Siasa

Kikwete: JPM amewazima midomo wapinzani ajenda ya rushwa

Spread the love

MWENYEKITI mstaafu Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jakaya Mrisho Kikwete amesema, Rais wa Tanzania anayemaliza muda wake, John Magufuli amewazima midomo wapinzani juu ya ajenda ya rushwa na ufisadi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Kikwete ameyasema hayo leo Jumamosi tarehe 17 Oktoba 2020 wakati anamuombea kura Rais Magufuli ambaye ni Mgombea Urais wa Tanzania kupitia CCM katika Uchaguzi Mkuu wa tarehe 28 Oktoba 2020 katika mkutano wa kampeni uliofanyika Uwanja wa Zakhiem-Mbagala Dar es Salaam.

Rais huyo mstaafu wa Tanzania wa Serikali ya awamu ya nne, amesema katika uongozi wa Rais Magufuli amefanikiwa kupambana na rushwa pamoja na kuanzisha Mahakama ya Mafisadi, kiasi kwamba wagombea wa upinzani wameshindwa kuitumia ajenda hiyo katika mikutano ya kampeni.

“Rais Magufuli kapambana na rushwa, mahakama ya mafisadi imeanzishwa ndio manaa uchaguzi huu sijasikia mgombea yeyote aliyezungumza rushwa na atakeyechukua kama ajenda atakua ameishiwa,” amesema Kikwete.

Kikwete amewaomba wananachi wa Temeke na Mbagala wamchague tena Rais Magufuli ili amalize kazi aliyoianza katika awamu yake ya kwanza ya uongozi, ikiwemo ujenzi wa vituo vya afya na hospitali, barabara, usambazaji maji na umeme na huduma nyingine za kijamii.

“Tumchague Magufuli aendelee kuongoza nchi yetu, tumpe miaka mitano mingine amalize ngwe yake. CCM ina sera nzuri za kudumisha masilahi ya kisiasa, kijamii, kitamaduni, kiusalama na watu wake. Hakuna chama kingine kinachofanana na CCM mimi sikijui,” amesema Kikwete.

Wakati huo huo, Kikwete amewaomba Watanzania kuchagua wagombea wa CCM akisema kwamba chama hicho kina sera nzuri zinazodumisha amani, umoja na muungano wa Taifa.

Pamoja na kuwa na Ilani zenye kutatua changamoto za Watanzania.

“Sera nzuri za CCM zimeliunganisha taifa la Tanzania, zimejenga umoja, udugu, upendo miongoni mwa watu na wananchi wa Tanzania. Sababu ya pili ya kutaka CCM ichaguliwe tena kuongoza nchi yetu, imekuwa inatengeneza ilani za uchaguzi zinazotambua changamoto zinazokabili wananchi wa Tanzania,” amesema Kikwete.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!