Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kikwete amtaka Samia kuwa mkali ‘usivumilie upuuzi’
Habari za SiasaTangulizi

Kikwete amtaka Samia kuwa mkali ‘usivumilie upuuzi’

Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete
Spread the love

RAIS mstaafu Dk. Jakaya Kikwete ameushauri uongozi mpya wa CCM unaongozwa na Mwenyekiti Dk Samia Suluhu Hassan kuwa wakali na kutovumilia maneno yanayokigawa chama hicho na badala yake watu wanaotoa kauli hizo waitwe kwenye maadili na kuonywa.

Pia amesema hamuoni Mwana CCM atakayechukua fomu kumpinga Samia katika uchaguzi mkuu mwaka 2025. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Dk. Kikwete ametoa kauli hiyo jana tarehe 8 Disemba 2022 wakati akihutubia mkutano wa 10 wa chama hicho uliofikia tamati jiji Dodoma.

Amesema ni ukweli uliodhahiri kwamba hapa Tanzania hakuna mwanasiasa maarufu kumshinda Rais Samia.

“Usisumbuliwe na maneno hayo. Ni waombe ndugu zangu acheni uongo. Ukiangalia huko mitandaoni kuna maneno mengi ya uongo, ni upuuzi tu… tuache hii tabia ndiyo inakigawa Chama chetu.

“Mnawafanya viongozi wetu wapate stress (jakamoyo) tu. Mkiwasikia watu wanasema maneno waiteni kwenye maadili na kama hana maelezo aambiwe aache uongo.

“Hii ndio njia pekee itakayo ondoa uchimbi. Chama chetu ni kikubwa sana hakistahili kuvumilia upuuzi kama huo. Mkiuvumilia Chama hiki kitavurugika kwa maslahi ya wapuuzi. Naomba muwe wakali,” amesema Dk. Kikwete.

3 Comments

  • Kuna ubaya gani kama mwana CCM anafiiria au anaota au anadokeza kuwa angependa naye kugombea urais mwaka 2025? Si haki yake ya kikatiba? Kwanini aitwe mpuuzi au msaliti? Katiba gani imesema Mama Samia hwezi kuwa na mgombea mwenzake? Acheni udikteta katika chama

  • Kama kuna upuuzi mkubwa ni ule wa Mzee Makamba kusema kuwa Kikwete hakufa kwa sababu ni mtu mzuri
    Kikwete badala ya kukanusha ameonekana akiche tu

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

error: Content is protected !!