RAIS mstaafu Dk. Jakaya Kikwete ameushauri uongozi mpya wa CCM unaongozwa na Mwenyekiti Dk Samia Suluhu Hassan kuwa wakali na kutovumilia maneno yanayokigawa chama hicho na badala yake watu wanaotoa kauli hizo waitwe kwenye maadili na kuonywa.
Pia amesema hamuoni Mwana CCM atakayechukua fomu kumpinga Samia katika uchaguzi mkuu mwaka 2025. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Dk. Kikwete ametoa kauli hiyo jana tarehe 8 Disemba 2022 wakati akihutubia mkutano wa 10 wa chama hicho uliofikia tamati jiji Dodoma.
Amesema ni ukweli uliodhahiri kwamba hapa Tanzania hakuna mwanasiasa maarufu kumshinda Rais Samia.
“Usisumbuliwe na maneno hayo. Ni waombe ndugu zangu acheni uongo. Ukiangalia huko mitandaoni kuna maneno mengi ya uongo, ni upuuzi tu… tuache hii tabia ndiyo inakigawa Chama chetu.
“Mnawafanya viongozi wetu wapate stress (jakamoyo) tu. Mkiwasikia watu wanasema maneno waiteni kwenye maadili na kama hana maelezo aambiwe aache uongo.
“Hii ndio njia pekee itakayo ondoa uchimbi. Chama chetu ni kikubwa sana hakistahili kuvumilia upuuzi kama huo. Mkiuvumilia Chama hiki kitavurugika kwa maslahi ya wapuuzi. Naomba muwe wakali,” amesema Dk. Kikwete.
Kuna ubaya gani kama mwana CCM anafiiria au anaota au anadokeza kuwa angependa naye kugombea urais mwaka 2025? Si haki yake ya kikatiba? Kwanini aitwe mpuuzi au msaliti? Katiba gani imesema Mama Samia hwezi kuwa na mgombea mwenzake? Acheni udikteta katika chama
Kama kuna upuuzi mkubwa ni ule wa Mzee Makamba kusema kuwa Kikwete hakufa kwa sababu ni mtu mzuri
Kikwete badala ya kukanusha ameonekana akiche tu
Wimbo wa Balisidya!
“Wema hawana maisha,
wema wanapozaliwa,
wema wanauwawa!”