Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kikokotoo chaondoka na Mkurugenzi SSRA
Habari za Siasa

Kikokotoo chaondoka na Mkurugenzi SSRA

Spread the love

RAIS John Magufuli ametengua uteuzi wa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) Dk. Irene Isaka. Anaripotu Yusuph Katimba…(endelea).

Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu imeeleza kuwa, Dk. Irene atapangiwa kazi nyingine.

Hatua hiyo imechukuliwa na Rais Magufuli muda mchache baada ya kufanya mkutano na wawakilishi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii, serikali na vyama vya wafanyakazi ambapo alionesha kutoridhishwa na mfumo mpya wa kikokotoo.

Mfumo wa awali ukiruhusu mstaafu kuchukua asilimia 50 kwa mkupuo kisha zilizobaki akiendela kupewa kidogo kidogo.

Mfumo wa Sasa ulijielekeza kutoa kwa mkupuo asilimia 25 jambo ambalo lilikuwa likilalamikiwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

error: Content is protected !!