Monday , 29 May 2023
Home Habari Mchanganyiko Kijiji Matinje kupelekewa mawasiliano
Habari Mchanganyiko

Kijiji Matinje kupelekewa mawasiliano

Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania, inakusudia kutatua matatizo ya mawasiliano Kijiji cha Matinje Ikombandulu, ambalo ni eneo la machimbo lenye idadi kubwa ya watu ili kurahisisha biashara eneo hilo. Anaripoti Jemima Samwel DMC…(endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo Jumatano, tarehe 2 Juni 2021, bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Kundo Mathew katika kipindi cha maswali na majibu wakati akiwa anajibu swali la Seif Khamis Gulamali mbunge wa Manonga (CCM).

Mathew amesema, Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote unatekeleza miradi mitatu katika Jimbo la Manonga.

“Miradi hiyo inatekelezwa katika Kata zaIgoweko(Mnara huu unahudumia pia Kata ya Uswaya), Sungwizi na Ngulu.Utekelezaji wa miradi katika kata hizi umekamilika.”

“Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) itakifanyia tathmini Kijiji cha Matinje Ikombandulu na hatimaye kijiji hiki kitaingizwa katika orodha ya vijiji vitakavyojumuishwa katika zabuni zitakazotangazwa katika mwaka wa fedha 2021/22,” amesema Mathew.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Kirigini kuzikwa leo Butiama

Spread the love  MWILI wa aliyekuwa Mbunge wa Musoma Vijijini (1980-1985), Herman...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jeshi la Polisi kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika utafiti

Spread the love  JESHI la Polisi Nchini limesema kuwa katika kukabiliana na...

Habari Mchanganyiko

Kampeni ya Samia Legal Aid yazinduliwa Manyara, kesi 45 zapokelewa

Spread the love  KAMPENI ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia, imezinduliwa...

Habari Mchanganyiko

NMB ya kwanza kuzindua Malipo kwa QR na UnionPay International

Spread the loveBENKI ya NMB kwa kushirikiana na UnionPay International (UPI), wamezindua...

error: Content is protected !!