Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Kijana mbaroni kwa kumbaka mama yake mzazi
Habari Mchanganyiko

Kijana mbaroni kwa kumbaka mama yake mzazi

Spread the love

 

MATUKIO ya ukosefu wa maadili mkoani Dodoma yamezidi kuutikisa mkoa huo baada ya Jeshi la Polisi mkoani humo kumnasa kijana mmoja mwenye umri wa miaka 30 kwa tuhuma za kumbaka mama yake mzazi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma …  (endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari leo tarehe 22 Disemba, 2021 Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma, Onesmo Lyanga amesema tukio hilo limetokea wilayani Kondoa.

Aidha, amesema katika operesheni waliyoifanya hivi karibuni pia walimkamata Babu mwenye umri wa miaka 61 kwa tuhuma za kumbaka mjukuu wake mwenye umri wa miaka 11.

Amesema mjukuu huyo anayesoma darasa la nne, wote pamoja na babu yake ni wakazi wa Kongwa.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma, Onesmo Lyanga

Pia ameongeza katika operesheni hiyo pia wamemkamata baba mwenye umri wa miaka 30 ambaye ametuhumiwa kumuingilia kinyume na maumbile mwanaye mwenye  umri wa miaka minne.

Amesema kutokana na matukio hayo ni dhahiri vitendo vya ukatili uliokithiri vimeendelea kushamiri mkoani humo hivyo ni vema jamii kurejea kwenye maadili.

“Lakini watuhumiwa wote tumeshawakamata na kwa ajili ya taratibu za kuwafikisha mahakamani,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!