Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Kijana aibuka mshindi nchini Austria
KimataifaTangulizi

Kijana aibuka mshindi nchini Austria

Sebastian Kurz
Spread the love

MKUU wa chama cha kihafidhina nchini Austria cha People’s Party, Sebastian Kurz, anaelekea kupata ushindi wa kuliongoza taifa hilo akiwa na umri mdogo, anaandika Hamis Mguta.

Kurz mwenye umri wa miaka 31 yupo katika nafasi nzuri ya kuunda serikali ya muungano.

Haijulikani wazi iwapo atafikiria kuunda serikali ya muungano na chama kinachopinga uhamiaji Freedom Party, kilichoibuka nafasi ya tatu katika uchaguzi huo.

Akihutubia wafuasi wake, Kurz amesema “Ni wakati wa kuleta mabadiliko katika nchi hii, leo ni siku muhimu kwetu kuibadilisha nchi hii na ninasema asante kwa wale waliowezesha hili”.

Kabla ya uchaguzi, Kurz alishika nafasi ya Waziri akiwa na umri mdogo, akitumia nafasi ya Waziri wa Mambo ya Kigeni barani Ulaya wakati huo akiwa na miaka 27.

Mwezi Mei mwaka 2017 akawa kiongozi wa chama cha People’s Party.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!