Friday , 9 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Kigogo wa TAKUKURU anaswa akipokea rushwa
Habari Mchanganyiko

Kigogo wa TAKUKURU anaswa akipokea rushwa

Spread the love

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (TAKUKURU) imemfukuza kazi Cosmas Batanyita, aliyekuwa Mchunguzi Mwandamizi wa taasisi hiyo, kwa kosa la kuomba na kupokea rushwa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Hayo amesema Kamishna wa Polisi Diwani Athumani, Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU wakati akizungumza na wanahabari leo tarehe 9 Agosti 2019 jijini Dar es Salaam.

Kamishna Athumani amesema Batanyita alikuwa mchunguzi mwandamizi katika makao makuu ya ofisi za TAKUKURU jijini Dar es Salaam.

“Tunapenda kuutarifu umma kuwa tumemkamata afisa wa TAKUKURU aitwaye Cosmas Revelian Batanyita, alikuwa mchunguzi mwandamizi makao makuu ya ofisi ya Dar es Salaam kwa kosa la kuomba na kupokea rushwa, na  amefukuzwa kazi,” amesema Kamishna Athumani.

Wakati huo huo, Kamishna Athumani amewaonya matapeli wanaojifanya maafisa wa TAKUKURU kujipatia fedha kutoka kwa wananchi, akisema kwamba taasisi hiyo imejipanga kukabiliana nao.

Kamishna Athumani amesema hivi sasa kuna wimbi la matapeli wanaojifanya ni maafisa wa TAKUKURU na vyombo vingine vya ulinzi na usalama, wanaotumia mbinu mbalimbali kuomba hongo kutoka kwa wananchi.

“Matapeli hawa wamekuwa wakitumia mbinu mbalimbali ikwia pamoja na kupigia simu wananchi wakitaka wapewe hongo ili wasichukuliwe hatua wakidai kuwa wanakabiliwa na makosa ya rushwa. Wale wote wanaotaka kuchafua taswira chanya ya TAKUKURU kuacha mara moja  tabia hiyo yenye lengo la kuondoa imani ya wananchi kwa serikali yao,” amesema Kamishna Athumani.

Aidha, Kamishna Athumani amewataka wananchi kuwa makini na watu wanaojitambulisha kwao kwamba ni maafisa wa TAKUKURU.

“Ni rai yangu kwenu, mwananchia usikubali kudanganywa na yeyote yule bila kumdadisi japo kwa kumtaka ajitambulishe kwako ikiwezekana akupatie kitambulisho ama akueleze kosa lako, hii ni haki.

TAKUKURU haifanyi kazi zake vichochoroni, afisa wa TAKUKURU hufanya kazi zake za kiuchunguzi huwa na kitambulisho pamoja  nayaraka anazopewa na ofisi kufanya upelelezi nje ya ofisi,” amesisitiza Kamishna Athumani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Askari Polisi zaidi ya 100 wapigwa msasa wa udereva kukabiliana na ajali

Spread the love  KATIKA kuhakikisha wimbi la ajali za barabarani zinapungua kama...

Habari MchanganyikoTangulizi

Serikali yakana kuhamisha kwa nguvu jamii ya Kimasai Loliondo

Spread the loveWAZIRI wa Katiba na Sheria nchini Tanzania, Dk. Damas Ndumbaro,...

Habari Mchanganyiko

Tunduma watenga 60 milioni kujenga machinjio ya kisasa

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma Imetenga kiasi cha Tshs Miloni 60...

Habari Mchanganyiko

Bilioni 17 kujenga bandari kavu Tunduma

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma iliyopo wilayani  Momba mkoani Songwe imepatiwa...

error: Content is protected !!