Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Kigogo wa Acacia kizimbani kwa utakatishaji fedha
Habari Mchanganyiko

Kigogo wa Acacia kizimbani kwa utakatishaji fedha

Spread the love

ASA Mwaipopo (55), Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni za Madini za Bulyanhulu, North Mara na Pangea zilizokuwa chini ya Acacia, amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa mashtaka tisa yanayomkabili ikiwemo utakatishaji fedha na kughushi, na kujipatia dola za marekani 840,000. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Mwaipopo amesomewa mashtaka hayo leo tarehe 23 Oktoba 2018 na Mawakili wa Serikali, Faraja Nchimbi na Jacqline Nyantori mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi.

Upande wa mashtaka umedai kuwa, Mwaipopo ametenda makosa hayo ya kula njama, kuongoza uhalifu wa kupangwa, kughushi, ukwepaji kodi na utakatishaji fedha, katika kipindi cha Aprili 11 mwaka 2018 na Juni 30 mwaka 2017.

Hata hivyo, kesi hiyo imeahirishwa hadi tarehe 31 Oktoba 2018 kutokana na upande wa mashtaka kutokamilisha upelelezi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Watendaji Kata, Mitaa watakaoshindwa kusimamia usafi kukiona

Spread the love  WATENDAJI wa kata, mitaa na vitongoji na maofisa afya...

Habari Mchanganyiko

Mtia nia urais TLS kukata rufaa kupinga kuenguliwa

Spread the love  MTIA nia ya kugombea Urais wa Chama cha Mawakili...

Habari Mchanganyiko

NBC yazindua kampeni ya mkeka wa ushindi na ATM zake

Spread the loveBENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imetangaza uzinduzi wa kampeni...

Habari Mchanganyiko

Uholanzi wampongeza Rais Samia kuimarisha vyombo vya habari, demokrasia

Spread the love  UBALOZI wa Uholanzi nchini Tanzania, umempongeza Rais Samia Suluhu...

error: Content is protected !!