Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Kigogo wa Acacia kizimbani kwa utakatishaji fedha
Habari Mchanganyiko

Kigogo wa Acacia kizimbani kwa utakatishaji fedha

Spread the love

ASA Mwaipopo (55), Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni za Madini za Bulyanhulu, North Mara na Pangea zilizokuwa chini ya Acacia, amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa mashtaka tisa yanayomkabili ikiwemo utakatishaji fedha na kughushi, na kujipatia dola za marekani 840,000. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Mwaipopo amesomewa mashtaka hayo leo tarehe 23 Oktoba 2018 na Mawakili wa Serikali, Faraja Nchimbi na Jacqline Nyantori mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi.

Upande wa mashtaka umedai kuwa, Mwaipopo ametenda makosa hayo ya kula njama, kuongoza uhalifu wa kupangwa, kughushi, ukwepaji kodi na utakatishaji fedha, katika kipindi cha Aprili 11 mwaka 2018 na Juni 30 mwaka 2017.

Hata hivyo, kesi hiyo imeahirishwa hadi tarehe 31 Oktoba 2018 kutokana na upande wa mashtaka kutokamilisha upelelezi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

error: Content is protected !!