Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Kigogo CUF asota rumande
Habari za SiasaTangulizi

Kigogo CUF asota rumande

Mjumbe wa Baraza Kuu la Uongozi la CUF Taifa, Abdallah Khatau
Spread the love

MJUMBE wa Baraza Kuu la Uongozi la CUF Taifa, Abdallah Khatau leo amefikisha siku ya tano akiwa rumande huku polisi wakigoma kumpa dhamana. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Licha ya kumnyima dhamana, Polisi wa Kituo cha Polisi cha Masasi mkoani Mtwara wamegomea ndugu zake kumuona Khatau.

Kwa mujibu wa ndugu wa karibu wa Khatau, Ebrahim Issally kupitia ukurasa wake wa Twitter jana tarehe 18 Januari 2019 aliandika kuwa, polisi hawajaeleza sababu za kukamatwa kwa Khatau pia wamegoma kuruhusu kumuona ndugu yao.

Naibu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mawasiliano na Umma CUF, Mbarala Maharagande amesema, hadi leo tarehe 19 Januari 2019, Khatau bado anashikiliwa na Jeshi la Polisi na kwamba, chama chake kinaendelea na jitihada za kushughulikia dhamana yake.

Alipoulizwa sababu za kukamatwa Khatau, Kamanda wa Polisi mkoani Mtwara, Blasius Chatanda alidai hana taarifa za kukamatwa kwa Khatau.

Pamoja na hivyo Kamanda Chatanda amesema, sio jambo rahisi kwa polisi kumkamata mtuhumiwa bila kueleza sababu.

Kamanda Chatanda ameshauri ndugu wa Khatau kwenda kwa Mkuu wa Upelelezi wa Wilaya ya Masasi (OCD), ili kujua sababu zilizopelekea Khatau kushikiliwa na Jeshi la Polisi.

“Sina taarifa hizo, ndio nasikia kutoka kwako, ila nitafuatilia taarifa hizo. Lakini haiwezekani polisi wamkamate bila ya kumwambia kosa. Kwa msaada wakamuone OCD,” amesema Kamanda Chatanda.

Khatau ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini CUF, alikamatwa tarehe 15 Januari 2019 akiwa nyumbani kwake wilayani Masasi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari MchanganyikoTangulizi

Afya ya akili yatajwa chanzo kuvunjika ndoa

Spread the loveCHANGAMOTO ya afya ya akili, imetajwa kuwa chanzo cha migogoro...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

error: Content is protected !!