Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kigogo Bavicha mbaroni kwa tuhuma za makosa mtandao
Habari za Siasa

Kigogo Bavicha mbaroni kwa tuhuma za makosa mtandao

Mratibu wa uhamasishaji wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha), Twaha Mwaipaya
Spread the love

 

MRATIBU wa uhamasishaji wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha), Twaha Mwaipaya, anadaiwa kukamatwa na Jeshi la Polisi mkoani Morogoro, kwa tuhuma za makosa ya kimtandao. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa ya tukio hilo imetolewa leo Ijumaa, Julai Mosi, 2022 na Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano Bavicha, Apolinary Boniface.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Mwaipaya amekamatwa jana tarehe 30 Juni 2022, mkoani Morogoro na kwamba leo asubuhi amesafirishwa kuelekea mkoani Dodoma, anakodaiwa kutekeleza makosa hayo.

“Bavicha tunalitaka Jeshi la Polisi mkoani Dodoma kumweleza Mwaipaya kosa analotuhumiwa nalo na kumwachia huru au kumpa dhamana kwa kuwa kosa wanalodai kumtuhumu nalo lina dhamana,” imesema taarifa ya Boniface.

MwanaHALISI Online ilipomtafuta kwa njia ya simu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma kuthibitisha taarifa hizo, simu yake iliita bila kupokewa. Jitihada za kumpata zinaendelea.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!