Tuesday , 5 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Kifo cha Rais Nkurunzinza, Magufuli atangaza maombolezo siku tatu
Habari Mchanganyiko

Kifo cha Rais Nkurunzinza, Magufuli atangaza maombolezo siku tatu

Spread the love

RAIS wa Tanzania, John Magufuli ametangaza maombolezo ya Kitaifa ya siku tatu kuanzia leo Jumamosi tarehe 13 hadi 15 Juni, 2020 kufuatia kifo cha Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Rais Nkurunzinza alifariki Jumanne tarehe 9 Juni 2020 kwa mshtuko wa moyo.

Taarifa iliyotolewa jana Ijumaa usiku tarehe 12 Juni 2020 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa imeeleza, katika kipindi chote cha siku tatu za maombolezo ya Kitaifa, bendera zote zitapeperushwa nusu mlingoti.

Rais Magufuli ameeleza, Tanzania inatoa heshima hiyo kwa kifo cha Pierre Nkurunziza kwa kutambua alikuwa Rais wa nchi jirani ambayo imekuwa na uhusiano na ushirikiano mzuri, wa kirafiki, kihistoria na kidugu na Tanzania.

“Burundi ni mwanachama mwenzetu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na Mhe. Rais Nkurunziza aliipenda Jumuiya hii.”

Rais John Magufuli

“Pia, aliipenda Tanzania na alishirikiana nasi kila ilipohitajika, hivyo nimeona Watanzania tuungane na ndugu zetu wa Burundi katika kuomboleza na kumkumbuka Rais Nkurunziza ambaye aliiona Tanzania kama nyumbani kwake” amesema Rais Magufuli.

Rais Magufuli amerudia kutoa pole kwa Mama Denise Bucumi, Mjane wa Rais Nkurunziza, familia, Serikali na Wananchi wote wa Burundi kwa kuondokewa na mpendwa wao na amemuombea kwa Mwenyezi Mungu aipumzishe roho yake mahali pema peponi, Amina.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

RPC Songwe awafunda trafki kuzingatia uadilifu

Spread the loveASKARI wa kikosi cha usalama barabarani mkoani Songwe wametakiwa kuendelea...

Habari Mchanganyiko

Mchimba madini jela maisha kwa kubaka, alihonga Sh 500

Spread the loveMahakama ya wilaya ya Songwe imemtia hatiani na kumhukumu kifungo...

Habari Mchanganyiko

Mlima wa Moto wazindua kongamano la SHILO kumuenzi Rwakatare

Spread the loveKANISA la Mlima wa Moto Mikocheni jijini Dar es Salaam,...

Habari MchanganyikoTangulizi

20 wafariki dunia kwa mafuriko Manyara

Spread the loveMVUA za vuli zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini zimeleta madhara...

error: Content is protected !!