Wednesday , 17 April 2024
Home Kitengo Maisha Burudika Kifo cha Magufuli, Majaliwa awashukuru wasanii
Burudika

Kifo cha Magufuli, Majaliwa awashukuru wasanii

Spread the love

 

WAZIRI mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa amewashukuru na kuwapongeza wasanii wote nchini waliojitoa kutunga nyimbo mbali mbali za kumuenzi aliyekuwa Rais wa Tanzania hayati Dk, John Magufuli. Anaripoti Matilda Peter…(endelea) 

Majaliwa ameyasema hayo hii leo tarehe 22 Machi, 2021 jijini Dodoma katika shughuli ya kitaifa ya kumuaga hayati Magufuli iliyofanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri.

Katika hotuba yake mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu na waombolezaji wengine, Majaliwa alishukuru kundi hilo la wasanii ambao mara baada ya hotuba hiyo kuisha waliimba wimbo maalumu wa maombolezo kwa alaiki iliyouzulia hapo.

Wasanii walioudhulia na kutumbuiza wimbo huo ni pamoja na Linah, Nandy, Marioo, Khadija kopa, Ben pol, Dogo janja, Jay melody, Stamina, Young Lunya, Goodluck Gosbert na mrisho mpoto.

Toka aliyekuwa makamu wa Rais Samia Suluhu kutangaza kifo cha Magufuli tarehe 17 Machi, 2021 nyimbo Zaidi ya 20 za maombolezo zilitungwa kutoka kwa wasanii wa ndani na nje ya nchi.

Majaliwa Kassim, Waziri Mkuu wa Tanzania akiaga mwili wa Hayati John Magufuli

Wasanii wengeni walioweza kuimba nyimbo ni pamoja na Harmonize, Rayvany, Rosaree, Nandy, Juma Jux, Shilole, Ommy dimpoz, Peter msechu, Kala jeremiah, One six, Zuchu, Alikiba, Marioo, Darassa, na Mzee yusuph

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BurudikaMichezo

Kizz Daniel aunguruma na EP mpya ‘Thankz alot’

Spread the loveMKALI wa muziki nchini Nigeria, Kizz Daniel ametoa EP yake...

BurudikaHabari za Siasa

Samia amchangia Professa Jay mil. 50, Chadema, wasanii wamwaga manoti

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amechangia kiasi cha Sh 50 milioni...

Burudika

Piga makofi kwa Mr. Eazi …achomoka na ‘The Evil Genius’

Spread the loveMAKOFI kwa Mr Eazi! Staa wa Afropop, Mr Eazi ameachia...

Burudika

Kishindo cha Afro B katika “Wo wo wo” akiwa na Rich the Kid&Rimzee

Spread the loveSTAA ambaye alitambulishwa na ngoma maarufu, Afrowave ‘Drogba’, Afro B,...

error: Content is protected !!