Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Kifo cha Loya, Zitto amlilia
Habari za Siasa

Kifo cha Loya, Zitto amlilia

zitto Kabwe, Kiongozi wa ACT-Wazalendo
Spread the love

 

MTENDAJI Mkuu wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD), Daniel Loya amefariki dunia asubuhi ya leo Jumatano, katika Hospitali ya Lugalo alikokuwa anapatiwa matibabu.

Taarifa ya kifo hicho imetolewa leo  tarehe 10 Februari 2021 na Zitto Kabwe, Mwenyekiti wa TCD.

Zitto ametuma salamu za pole kwa familiya ya Loya, na vyama wanachama wa TCD, ikiwemo Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Chama Cha Mapinduzi (CCM), Chama cha Wananchi (CUF), na ACT-Wazalendo.

“Mtendaji Mkuu wa TCD Bwana D. Loya amefariki dunia leo asubuhi katika hospitali ya Lugalo.

“Nikiwa Mwenyekiti wa TCD, natoa pole kwa familia ya ndugu Loya na kwa viongozi wote  wa vyama wanachama wa TCD, Chadema, CCM, CUF na ACT-Wazalendo,” ameandika Zitto katika ukurasa wake wa Twitter.

Mwenyekiti huyo wa TCD amesemaTanzania imepoteza mwanademokrasia wa dhati “tumepoteza mwanadekrasia wa dhati.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!