Tuesday , 30 May 2023
Home Habari Mchanganyiko Kibonde kuzikwa Jumamosi
Habari Mchanganyiko

Kibonde kuzikwa Jumamosi

Spread the love

MAZISHI ya aliyekiwa mtangazaji wa Kituo cha Redio Clouds, Ephrahim Kibonde atazikwa Jumamosi wiki hii. Anaripoti Bupe Mwakiteleko … (endelea).

Mwili wa Kibonde unatarajiwa kuwasili jijini Dar es Salaam leo Alhamisi Machi 7, saa nne usiku katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere na kuzikwa Jumamosi.

Joseph Kusaga, Mkurugenzi Mtendaji wa Clouds Media Group ametoa taarifa hiyo leo tarehe 7 Machi 2019 na kwamba, mwili wa Kibonde unatarajiwa kutua Dar es Salaam saa 4 usiku wa leo.

Amesema, baada ya kufika mwili huo utahifadhiwa katika Hospitali ya Jeshi Lugalo.

“Jana usiku niliongea na daktari Derrick aliyekuwa anamtibu Ephraim Kibonde akanihakikishia kuwa anaendelea vizuri lakini bahati mbaya wakati tunajiandaa kurudi Dar es Salaam hali ikabadilika na kusabaisha kifo chake.

“Taratibu za mazishi na maombolezo, zinafanyika nyumbani kwake Mbezi na tunatarajia kuaga na kumpumzisha siku ya Jumamosi katika makaburi ya Kinondoni karibu na kaburi la mke wake,” amesema Kussaga.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wenye ulemavu waiomba MISA-TAN iwajengee uwezo wa uhuru wa kujieleza

Spread the love  TAASISI ya vyombo vya Habari kusini mwa Afrika (MISA-TAN)...

Habari Mchanganyiko

Wanawake wajawazito 2000 Korogwe washiriki Marathon, Mwenyekiti UWT amsifu Jokate

Spread the loveWANAWAKE wajawazito zaidi ya 2000 wilayani Korogwe mkoani Tanga wameshiriki...

Habari Mchanganyiko

Kirigini kuzikwa leo Butiama

Spread the love  MWILI wa aliyekuwa Mbunge wa Musoma Vijijini (1980-1985), Herman...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jeshi la Polisi kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika utafiti

Spread the love  JESHI la Polisi Nchini limesema kuwa katika kukabiliana na...

error: Content is protected !!