Friday , 29 March 2024
Habari za Siasa

Kibatala amnasua Sugu

Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi-Mbeya imewaachia kwa dhamana washtakiwa Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi na Katibu wa Chadema Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Emmanuel Masonga katika kesi. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Watuhumiwa hao wanashtakiwa kwa kosa kutumia lugha ya fedheha kwa Rais John Magufuli ambapo walinyimwa dhamana kutokana upande wa jamhuri kupinga dhamana yao mahakamani hapo.

Leo wakili wa utetezi Peter Kibatala aliieleza mahakama kuwa upande wa Jamhuri hauna hoja za kuendelea kushikilia dhamana ya watuhumia kutokana na kufunga pazia la ushahidi mahakamani.

Upande wa Jamhuri umewasilisha mashahidi sita mahakamani hapo.

Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo Michael Mteite, amewapa dhamana watuhumiwa hao.

Watuhumiwa hao walijidhamini wenyewe kwa kusaini hati ya Sh. Milioni tano kila mmoja.

Mawakili wa pande zote mbili walikubaliana kuwasilisha majumuisho ya shauri hilo tarehe 19 Februari.

Kesi hiyo itatajwa tena Februari 26 mwaka huu ambapo mahakama hiyo itatoa hukumu ya kwamba Sugu na mwenzie wana hatia au laa.

Kama mahakama itawakuta na hatia watuhumiwa hao wanalazima kujitetea kama haikujiridhisha kuhusu tuhuma hizo itawaachia huru.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!