SERIKALI ya Tanzania, imeokoa Sh.132.24 bilioni, baada ya kushinda kesi mbalimbali za ndani na nje ya nchi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Hayo yamesemwa na Profesa Palamagamba Kabudi, Waziri wa Katiba na Sheria, leo Jumatano, tarehe 28 Aprili 2021, wakati akiwasilisha bajeti ya wizara yake bungenji jijini Dodoma yam waka 2021/22.
Amesema, Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali, imeendelea kujenga uwezo wa kitaasisi katika kuratibu, kusimamia na kuendesha mashauri ya madai na usuluhishi kwa kuhakikisha maslahi ya Taifa yanazingatiwa wakati wa uendeshaji wa mashauri hayo.
Profesa Kabudi amesema, katika kipindi cha Julai, 2020 hadi Machi, 2021, ofisi ilianza na mashauri ya madai 3,111 ya kitaifa na kusajili mashauri mapya 545 na kuwa na jumla ya mashauri 3,656.
“Katika kipindi hicho, mashauri 418 yamemalizika na 3,238 yapo katika hatua mbalimbali za usikilizwaji,” amesema Profesa Kabudi.
Amesema, wizara kupitia, Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali, ilikuwa na mashauri ya madai ya kimataifa 20, kati ya hayo, mashauri manne yamemalizika na 16 yanaendelea kufanyiwa kazi.
“Katika kuendesha mashauri hayo ya madai ya kitaifa na kimataifa, Serikali imeokoa kiasi cha Sh.132.24 bilioni ambacho kingelipwa kwa wadai endapo Serikali ingeshindwa kesi hizo,” amesema
Leave a comment