Thursday , 18 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kesi ya Zitto Kabwe yaiva
Habari za Siasa

Kesi ya Zitto Kabwe yaiva

Zitto Kabwe akitinga mahakamani Kisutu
Spread the love

UPANDE wa Mashtaka katika mashauri matatu ya uchochezi yanayomkabili Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, umekamilisha upelelezi wa mashauri hayo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Wakili wa Serikali Mwandamizi, Mutalemwa Kishenyi leo tarehe 26 Novemba 2018 mbele ya Hakimu, Huruma Shahidi amedai kwamba upelelezi wa shauri hilo umekamilika.

Baada ya maelezo hayo ya upande wa mashtaka, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imepanga tarehe 13 Desemba mwaka huu kuwa siku ya kumsomea maelezo ya awali (PH), Zitto.

Upande wa utetezi ukiongozwa na wakili Peter Kibatala ulidai kuwa hauna pingamizi juu ya tarehe hiyo.

Zitto anadaiwa kutenda makosa hayo tarehe 28 Oktoba 2018 katika mkutano wake na waandishi wa habari uliofanyika jijini Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia kutunukiwa udaktari wa heshima Uturuki

Spread the loveBaraza la Chuo Kikuu cha Ankara, ambacho ni cha pili...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia atua Uturuki kwa ziara ya siku 5

Spread the loveRais Samia Suluhu Hassan leo Jumatano amewasili nchini Uturuki kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Samia arejesha mikopo ya 10%, bilioni 227.96 zatengwa

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amerejesha utaratibu wa utoaji mikopo...

Habari za Siasa

Rais Samia amfariji mjane wa Musa Abdulrahman

Spread the loveRais Samia Suluhu Hassan leo Jumanne amempa pole Mwanakheri Mussa...

error: Content is protected !!