Wednesday , 27 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Kesi ya Zitto Kabwe yaiva
Habari za Siasa

Kesi ya Zitto Kabwe yaiva

Zitto Kabwe akitinga mahakamani Kisutu
Spread the love

UPANDE wa Mashtaka katika mashauri matatu ya uchochezi yanayomkabili Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, umekamilisha upelelezi wa mashauri hayo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Wakili wa Serikali Mwandamizi, Mutalemwa Kishenyi leo tarehe 26 Novemba 2018 mbele ya Hakimu, Huruma Shahidi amedai kwamba upelelezi wa shauri hilo umekamilika.

Baada ya maelezo hayo ya upande wa mashtaka, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imepanga tarehe 13 Desemba mwaka huu kuwa siku ya kumsomea maelezo ya awali (PH), Zitto.

Upande wa utetezi ukiongozwa na wakili Peter Kibatala ulidai kuwa hauna pingamizi juu ya tarehe hiyo.

Zitto anadaiwa kutenda makosa hayo tarehe 28 Oktoba 2018 katika mkutano wake na waandishi wa habari uliofanyika jijini Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

Habari za SiasaTangulizi

Mgawo wa umeme: Rais Samia ampa miezi sita bosi mpya TANESCO

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amempa miezi sita Mkurugenzi...

Habari za Siasa

Rais Samia avunja bodi ya REA

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Balozi Jacob Kingu, kuwa...

error: Content is protected !!