Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Kesi ya uvamizi: Sheikh Ponda arudishwa kortini
Habari MchanganyikoTangulizi

Kesi ya uvamizi: Sheikh Ponda arudishwa kortini

Sheikh Issa Ponda, Katibu wa Taasisi na Jumuiya za Kiislamu
Spread the love

SHEIKH Ponda Issa Ponda, Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, leo tarehe 11 Juni 2019 anapandishwa kizimbani kwenye Mahakama ya Rufani, jijini Dar es Salaam baada ya serikali kumkatia rufaa. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Kiongozi huyo wa Kiislam, anapandishwa tena kizimbani kusikiliza rufaa katika Mahakama ya Rufaa baada ya serikali kutoridhishwa na uamuzi wa Mahakama Kuu kumfutia hukumu ya Mahakama ya Kisutu katika kesi ya jinai namba 245 ya 2012.

Jaji Augustine Shangwa wa Mahakama Kuu, tarehe 27 Novemba 2014 alifuta hukumu iliyotolewa na Mahakaka ya Kisutu iliyomtia hatiani Sheikh Ponda, kwenye kesi yake ya uvamizi wa kiwanja cha Markaz kilichopo Chang’ombe jijini Dar es Salaam.

Katika kesi hiyo iliyokuwa ikimkabili na wenzake 49, Mahakama ya Kisutu ilimtia hatiani Sheikh Ponda kwa kosa la kuingia kijinai katika eneo la ardhi ya Kampuni ya Agritanza Ltd, eneo la Chang’ombe Markazi, eneo ambalo lilikuwa likimilikiwa na Waislam.

Pamoja na Mahakama ya Kisutu tarehe 9 Mei 2013 chini ya Hakimu Mkazi Victoria Nongwa kumtia hatiani Sheikh Ponda, mahakama hiyo ilimwachia huru huku ikimpa sharti la kutotenda kosa lolote katika kipindi cha miezi 12 kwa mujibu wa kifungu ncha 25 (g) cha Sheria ya Kanuni za Adhabu.

Sheikh Ponda kupitia wakili wake Juma Nassoro, alikata rufaa hukumu hiyo katika Mahakama Kuu akieleza kutokubaliana nayo. Mahakama Kuu ilitengua hukumu hiyo na kumwacha Sheikh Ponda huru bila masharti yoyote.

Hata hivyo, serikali ilikata rufaa katika Mahakama ya Rufani kupinga hukumu ya Mahakama Kuu, leo Sheikh Ponda atasimama mahakamani hapo ili kusikiliza rufaa hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

error: Content is protected !!