Tuesday , 26 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Kesi ya Mbunge Kubenea kunguruma Septemba 4
Habari za Siasa

Kesi ya Mbunge Kubenea kunguruma Septemba 4

Saed Kubenea, Mbunge wa Ubungo (Chadema)
Spread the love

MAHAKAMA ya Wilaya ya Dodoma imepiga kalenda kesi ya Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea (Chadema) hadi Septemba 4 mwaka huu kutokana na uchunguzi wa kesi hiyo kutokamilika, anaandika Dany Tibason.

Kubenea anashtakiwa kwa kosa la jinai ambalo anadaiwa kumshambulia mbunge wa viti maalum (CCM), Juliana Shonza wakati wa bunge la bajeti.

Hakimu James Karayemaha alipanga tarehe hiyo na wakili wa serikali Phobie Magili, alikubaliana naye hivyo kesi hiyo itaendelea Septemba 4, mwaka huu.

Awali Kubenea alisema utaratibu wa kisheria uliotumika siyo mzuri hivyo ni vyema kesi hiyo ingebaki polisi hadi hapo upepelezi utakapokamilika na kwamba ni matumizi mabaya ya rasilmali za serikali.

Naye wakili anayemtetea mshitakiwa Kubenea, Isaac Mwaipopo amesema kuwa wao bado wanasubiria upelelezi ukamilike kwani wana imani na mahakama.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia avunja bodi ya REA

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Balozi Jacob Kingu, kuwa...

Habari za SiasaTangulizi

Chande aliyeng’olewa TANESCO kwenda TTCL apelekwa Posta

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua aliyekuwa, Mkurugenzi Mkuu wa...

Habari za Siasa

Kamugisha aanika utekelezaji mpango kazi 2022/23

Spread the loveMWENYEKITI wa Ngome ya Vijana ya Chama Cha ACT-Wazalendo Mkoa...

Habari za Siasa

Vijana ACT-Wazalendo wakabidhiwa kivumbi kulinda kura uchaguzi 2024,2025

Spread the loveNGOME ya Vijana ya Chama cha  ACT-Wazalendo, imetakiwa kuwanoa wafuasi...

error: Content is protected !!