Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kesi ya Mbowe: Serikali kutumia mashahidi 24, vielelezo 19
Habari za SiasaTangulizi

Kesi ya Mbowe: Serikali kutumia mashahidi 24, vielelezo 19

Freeman Mbowe akiwasili mahakamani Kisutu
Spread the love

 

UPANDE wa mashtaka katika kesi inayomkabili Kiongozi wa chama kikuu kikuu cha upinzani nchini Tanzania cha Chadema, Freeman Mbowe na wenzake watatu umepanga kutumia mashahidi 24 na vielelezo vya maandishi 19. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Mbowe na wenzake watatu, Halfan Bwire Hassan, Adam Hassan Kasekwa na Mohamed Abdallah Ling’wenya wamesomewa maelezo ya awali ya tuhuma zinazowakabili ya uhujumu uchumi na kupanga njama za ugaidi leo Jumatatu, tarehe 23 Agosti 2021, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam.

Wakili wa Serikali Mwandamizi, Nassoro Katuga ameieleza mahakama hiyo mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Thomas Simba kwamba watatumia mashahidi 24 na vilelezo vya maandishi 19 katika Mahakama Kuu Kitengo cha Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi

Amesema, miongoni mwa mashahidi ni wanasheria wa kampuni za simu za Tigo na Airtel ambao waliotoa taarifa za miamala ya fedha kutoka kwa Mbowe kwenda kwa watu wakiwemo washtakiwa wenzake.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI TV, MwanaHALISI online na mitandao yetu ya kijamii kwa habari na taarifa mbalimbali

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!