Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Kesi ya Mbowe na wenzake yahairishwa
Habari za Siasa

Kesi ya Mbowe na wenzake yahairishwa

Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi imeipiga karenda kesi inayowakabili viongozi waandamizi tisa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) akiwemo Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho, mpaka Septemba 27 mwaka huu. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Watuhumiwa kwenye kesi hiyo ni pamoja na Freeman Mbowe Mwenyekiti wa Chadema, Vicent Mashinji Katibu wa Chadema, Halima Mdee, Mbunge Kawe John Mnyika Mbunge wa Kibamba na Easter Bulaya Mbunge wa Bunda. Salum Mwalimu Naibu Katibu Zanzibar.

Wengine ni Mchungaji Peter Msigwa Mbunge wa Iringa Mjini, Easter Matiko Tarime Mjini na John Heche Mbunge wa Tarime Vijijini.

Usikilizwaji wa kesi hiyo ulipangwa uanze leo Jumatatu Agosti 27, imeahirishwa baada ya mshtakiwa nambari tano, Ester Matiko kukosekana mahakamani.

Mdhamini wa Matiko ambae ni Diwani wa Gongo la Mboto, Dorcas Lukiko ameieleza Mahakama kuwa Matiko anaumwa na ameshauriwa na daktari wake apumzike.

Sambamba na kukosekana kwa Matiko, mshtakiwa namba mbili wa kesi hiyo, Peter Msigwa alimuomba Hakimu Mashauri ampatie muda wa wiki tatu ili atafute Wakili baada ya Wakili wake wa awali, Jeremia Mtobesya kujitoa kwenye kesi hiyo akimlaumu Hakimu Mashauri kukiuka baadhi ya taratibu za uendeshaji wa kesi.

Akiahirisha kesi, Mashauri aliwataka washtakiwa wote wafike bila kukosa siku iliyopangwa ya kuanza kusikilizwa kwa kesi hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!