Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kesi ya Mbowe na wenzake yahairishwa
Habari za Siasa

Kesi ya Mbowe na wenzake yahairishwa

Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi imeipiga karenda kesi inayowakabili viongozi waandamizi tisa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) akiwemo Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho, mpaka Septemba 27 mwaka huu. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Watuhumiwa kwenye kesi hiyo ni pamoja na Freeman Mbowe Mwenyekiti wa Chadema, Vicent Mashinji Katibu wa Chadema, Halima Mdee, Mbunge Kawe John Mnyika Mbunge wa Kibamba na Easter Bulaya Mbunge wa Bunda. Salum Mwalimu Naibu Katibu Zanzibar.

Wengine ni Mchungaji Peter Msigwa Mbunge wa Iringa Mjini, Easter Matiko Tarime Mjini na John Heche Mbunge wa Tarime Vijijini.

Usikilizwaji wa kesi hiyo ulipangwa uanze leo Jumatatu Agosti 27, imeahirishwa baada ya mshtakiwa nambari tano, Ester Matiko kukosekana mahakamani.

Mdhamini wa Matiko ambae ni Diwani wa Gongo la Mboto, Dorcas Lukiko ameieleza Mahakama kuwa Matiko anaumwa na ameshauriwa na daktari wake apumzike.

Sambamba na kukosekana kwa Matiko, mshtakiwa namba mbili wa kesi hiyo, Peter Msigwa alimuomba Hakimu Mashauri ampatie muda wa wiki tatu ili atafute Wakili baada ya Wakili wake wa awali, Jeremia Mtobesya kujitoa kwenye kesi hiyo akimlaumu Hakimu Mashauri kukiuka baadhi ya taratibu za uendeshaji wa kesi.

Akiahirisha kesi, Mashauri aliwataka washtakiwa wote wafike bila kukosa siku iliyopangwa ya kuanza kusikilizwa kwa kesi hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!