Tuesday , 30 May 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Kesi ya Mbowe: Mawakili wavutana, mahakama yarudia kutazama video
Habari za SiasaTangulizi

Kesi ya Mbowe: Mawakili wavutana, mahakama yarudia kutazama video

Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, imeamua kutazama upya ushahidi wa video iliowasilishwa na shahidi namba sita wa Jamhuri (koplo Charles), katika kesi ya uchochezi inayomuhusu Freeman Mbowe na wenzake. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea). 

Mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu wa mahakama hiyo Thomas Simba leo tarehe 20 Agosti 2019, mahakama hiyo imekubali video hiyo ioneshwe tena baada ya Wakili upande wa utetezi, Peter Kibatala kuomba ushahidi huo wa video urejewe akidai kuwa, Koplo Charles ameomba kwa zaidi ya mara nne kuuangalia kwa ajili ya kupata kumbukumbu ya maneno yaliyozungumzwa ndani yake.

Ombi hilo la Kibatala liliibuka mahakamani hapo, baada ya shahidi huyo kuieleza mahakama hiyo mara kadhaa, kwamba hakumbuki baadhi ya maneno na matukio yaliyoonekana katika ushahidi huo wa video.

Baada ya ombi hilo, Hakimu Simba alikubali ushahidi huo urejewe tena na kuiahirisha kesi hiyo kwa muda ili zoezi hilo lifanyike na kisha usikilizwaji wa kesi hiyo uendelee.

Jana tarehe 19 Agosti 2019 mahakama hiyo ilioneshwa kielelezo namba tano cha ushahidi wa video inayowaonesha washtakiwa hao tisa ambao ni viongozi wa Chadema akiwemo Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa chama hicho Taifa na Dk. Vicent Mashinji, Katibu Mkuu wa Chadema wakihutubia kwenye mkutano wa kufunga kampeni za uchaguzi wa marudio wa jimbo la kinondoni uliofanyika kwenye viwanja vya Buibui Kinondoni tareje 16 Februari 2018.

Pia, sehemu ya video hiyo hasa kipengele cha mwisho inaonesha watu kadhaa ikiwemo wafuasi wa Chadema wakiandamana kuelekea katika ofisi ya msimamizi wa uchaguzi wilaya ya Kinondoni.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online kwa taarifa zaidi kuhusu muendelezo wa usikilizwaji wa kesi hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jeshi la Polisi kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika utafiti

Spread the love  JESHI la Polisi Nchini limesema kuwa katika kukabiliana na...

KimataifaTangulizi

Mtuhumiwa wa mauaji ya halaiki ya Rwanda akamatwa Afrika Kusini

Spread the love  MMOJA wa watuhumiwa wakuu wa mauaji ya Kimbari ya...

Habari za Siasa

Musoma Vijijini waomba ujenzi wa barabara uanze haraka

Spread the loveJIMBO la Musoma Vijijini, mkoani Mara, limeomba Serikali kuhakikisha ujenzi...

error: Content is protected !!